Na Mary Gwera, Mahakama

Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Miradi ya Utawala Bora kutoka Benki ya Dunia (WB), Bi. Nicola Smithers ameipongeza Mahakama kwa utekelezaji wake wa Mradi wa Maboresho wa huduma za Kimahakama.

Bi. Smithers aliyasema hayo mapema Machi 19, alipokutana na Mhe. Jaji Mkuu ofisini kwake Mahakama ya Rufani-Dar es Salaam ambapo alipata nafasi ya kuongea na Mhe. Jaji Mkuu na Viongozi wengine wa Mahakama akiwemo Mtendaji Mkuu na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

“Nimefurahishwa na maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Maboresho ya huduma za Mahakama unaofadhiliwa na Benki ya Dunia, hususani katika eneo la uondoshaji wa mlundikano wa mashauri,” alisema Bi. Smithers

Akimkaribisha ofisini kwake, Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahimu Juma alimueleza Bi. Smithers juu ya maboresho mbalimbali yanayoendelea kufanyika ndani ya Mahakama ya Tanzania yote yakiwalenga wananchi ambao ndio wateja wa Mahakama.

“Miongoni mwa maeneo ambayo tunayoendelea kupambana nayo ili kurejesha imani ya wananchi kwa Mahakama ni pamoja na Rushwa, katika hili tmefanya jitihada kadhaa ikiwa ni pamoja na kusambaza mabango ‘posters’ yenye ujumbe wa kupinga rushwa na kuyasambaza katika ofisi za Mahakama kote nchini pamoja na kusambaza simu za kuwawezesha wananchi wenye malalamiko kutuma meseji ili malalamiko yao yaweze kufanyiwa kazi,” alieleza Mhe. Jaji Mkuu.
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Miradi ya Utawala Bora kutoka Benki ya Dunia (WB), Bi. Nicola Smithers akisaini Kitabu cha Wageni pindi alipowasili ofisini kwa Mhe. Jaji Mkuu wa Tanzania, Mahakama ya Rufani-Dar es Salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahimu Juma akiongea jambo na Mgeni wake Bi. Nicola Smithers ambaye ni Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Miradi ya Utawala Bora kutoka Benki ya Dunia (WB).
Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga (wa pili kushoto) akichangia jambo katika Mazungumzo hayo, wa kwanza kushoto ni Msajili Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revokati, wa pili kulia ni Meneja kutoka Benki ya Dunia-Tanzania, Bw. Dennis Biseko.
Msajili Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revokati (wa kwanza kushoto) akichangia jambo
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Miradi ya Utawala Bora kutoka Benki ya Dunia (WB), Bi. Nicola Smithers akizungumza jambo.
Mkuu wa Kitengo cha Maboresho-Mahakama, Mhe. Zahra Maruma akiwa katika mazungumzo hayo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...