Mkazi wa kata ya Kakonyo, Wilaya ya Missenyi mkoani Kagera ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM Bwana Faraja Kaijage akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili na Utalii jinsi alivyopigwa na kuumizwa na wafugaji wa nchini Uganda kwa kosa la kukamata mifugo ya waganda iliyokula mazao ya wananchi wa Tanzania katika kijiji hicho mwaka 2016 (Picha na Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi).
Na. Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii,
Mheshimiwa Nape Nnauye ameishauli Serikali kuboresha mipaka ya nchi
kwa wakati ili kuondokana na migogoro inayojitokeza mara kwa mara
kufuatia uvamizi wa wahamiaji kutoka nchi jirani.
Ameyasema hayo katika ziara ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge, Ardhi, Maliasili na Utalii ilipotembea mipaka kati ya Tanzania na
Uganda Wilaya ya Missenyi upande wa Tanzania Mkoa wa Kagera na
Wilaya ya Isingiro upande wa Uganda.
Nape amesema suala la kulinda mipaka ni muhimu hivyo ni vyema serikali
kupitia Wizara ya Ardhi ikatenga fedha za kutengeneza barabara zilizoko
mipakani ili kurahisisha ulinzi na usalama wa mipaka yetu na kuwezesha
wakazi wa nchi hizi mbili kutambua mipaka ili kuepusha migogoro ya
matumizi ya ardhi.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi, Maliasili na Utalii wakikagua mpaka wa Tanzania na Uganda katika eneo la mto kagera.
“Tumebaini kuwa kuingia kwa wananchi wa Uganda hasa kuleta mifugo
yao katika lanchi ya Missenyi kunachangiwa na kutokuwepo njia maalumu
na alama maalumu zinazotenganisha kati ya nchi na nchi hivyo watu
wanaingia kupitia katika vichochoro visivyo rasmi na kuhatarisha amani
kwa wakazi wa mipakani alisema Nnauye”
Kamati hiyo pia ilifanikiwa kufika katika vijiji vya Rwengiri, Bwenkoma na
Bubale vilivyopo kata ya Kakunyu na kubaini kuwa baadhi ya alama
zilizowekwa mpakani zimepotea hivyo wafugaji kutoka maeneo mbalimbali
wanaendelea na shughuli za ufugaji bila kujali sheria.
Mkuu wa wilaya ya Missenyi Kanali Denice Mwila amesema kuwa kamati
ya ulinzi na usalama imekuwa ikikagua mipaka na kutatua changamoto
mbalimbali hivyo kama barabara itatengenezwa katika mipaka yote ya
Missenyi kazi ya kuwabaini waarifu itakuwa rahisi.
Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Dkt. James Mtamakaya akiwaonesha Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili na Utalii mipaka iliyopo kati ya Tanzania na Uganda.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Dkt.
Angeline Mabula amesema kuwa mpaka sasa Wizara imepokea shilingi
bilioni 4 za kuimarisha mipaka ambapo fedha zitakazotumika kuimarisha
mpaka wa Tanzania na Uganda ni shilingi Bilioni 1.9 na shilingi Bilioni 2.1
kwa mpaka wa Tanzania na Kenya.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...