Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
JUKWAA la Lishe Tanzania(Panita) limeishauri Serikali kuhakikisha inaendelea kutoa elimu kuhusu lishe kwenye jamii ya Watazania ili kuwa na taifa lenye uwezo wa kujituma na kuleta maendeleo.

Ushauri huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Meneja wa Program wa Panita, Jane Msagati wakati anazungumza na Wahariri wa vyombo vya habari nchini kuhusu lishe bora.

Amesema kuna kila sababu ya kuhakikisha suala la lishe linapewa kipaumbele nchini kwa jamii kupata elimu itakayosaidia kutambua umuhimu wa lishe bora katika Taifa.

"Ukosefu wa lishe bora mwilini unasababisha udumavu na utapiamlo na matokeo yake husababisha magonjwa ambayo ni gharama kuyatibu na wakati mwingine husababisha ulemavu wa kudumu.

"Tatizo la lishe chini limesababisha kuongozeka kwa watoto wenye udumavu wa mwili na akili.Serikali inatumia fedha nyingi kugharamia matibabu, na hiyo ni hasara kubwa,"amesema Msagati.
Akizungumza kuhusu lishe  amesema ni msingi wa maendeleo kwa wote na jamii ihakikishe watoto wote wanapata lishe sahihi hususani siku 1000 za kwanza.

Pia amesema wababa wahusike kwenye malezi ya watoto na jamii ihakikishe kaya zinauhakika wa chakula kwa kuzalisha vyakula vya kutosha na kutotumia vyakula vyote kutengeneza pombe.

Amezungumzia umuhimu wa jamii kutengeneza bustani ndogondogo kuzunguka nyumba, bustani makasha/viroba kwa ajili ya mboga za majani.Pia kufuga wanyama wadogo kama kuku na  sungura.

Amesema ukosefu wa virutubisho mwilini husababisha njaa iliyojificha ambayo huchangia kwa kiwango kikubwa katika kusababisha magonjwa na vifo hususani kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano na akina mama walio katika umri wa kuzaa

Kuhusu mafunzo ya lishe kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini, Msagati amesema wanatambua nafasi ya vyombo vya habari katika kuelimisha umma.

Msagati amesema wahariri wa vyombo vya habari ndio wenye jukumu la kupitisha habari kwenye vyombo vyao na hivyo kukutana kati ya Panita na wahariri hao kutatoa fursa ya kuelezea umuhimu wa kuzipa kipaumbele habari za lishe bora.

Mhariri wa Gazeti la Mtanzania, Bakari Kimwanga na Mgariri wa Jarida la Afya na Ajira kutoka Gazeti la Mwananchi, Lilian Timbuka wamezungumzia umuhimu wa mafunzo yaliyotolewa na Panita kuhusu lishe bora na kwamba watatumia vyombo vyao kuwa mabalozi wa kuhamasisha jamii kuzingatia lishe bora.
Meneja wa Program wa Jukwaa la Lishe Tanzania(Panita), Jane Msagati akitoa mada kwenye semina ya wahariri wa vyombo vya habari iliyofanyika leo Dar es Saalam leo Semina hiyo ilikuwa inangumzia umuhimu wa lishe bora kwa jamii.
Mwandishi Mwandamizi wa Mlimani TV, Annuary Mkama akitoa somo kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini.
Wahariri na waandishi wa habari wakisikiliza mtoa mada katika semina la lishe bora kutoka kwa Meneja wa Programu wa Panita Jane Msagati(hayupo pichani).
Mtaalam wa masuala ya lishe kutoka Jukwaa la Lishe Tanzania(Panita), Deborah Esam akitoa mada kwa wahariri wa vyombo vya habari kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa jamii.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...