Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
JUKWAA
la Lishe Tanzania(Panita) limeishauri Serikali kuhakikisha inaendelea
kutoa elimu kuhusu lishe kwenye jamii ya Watazania ili kuwa na taifa
lenye uwezo wa kujituma na kuleta maendeleo.
Ushauri
huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Meneja wa Program wa Panita,
Jane Msagati wakati anazungumza na Wahariri wa vyombo vya habari nchini
kuhusu lishe bora.
Amesema
kuna kila sababu ya kuhakikisha suala la lishe linapewa kipaumbele
nchini kwa jamii kupata elimu itakayosaidia kutambua umuhimu wa lishe
bora katika Taifa.
"Ukosefu
wa lishe bora mwilini unasababisha udumavu na utapiamlo na matokeo yake
husababisha magonjwa ambayo ni gharama kuyatibu na wakati mwingine
husababisha ulemavu wa kudumu.
"Tatizo
la lishe chini limesababisha kuongozeka kwa watoto wenye udumavu wa
mwili na akili.Serikali inatumia fedha nyingi kugharamia matibabu, na
hiyo ni hasara kubwa,"amesema Msagati.
Akizungumza
kuhusu lishe amesema ni msingi wa maendeleo kwa wote na jamii
ihakikishe watoto wote wanapata lishe sahihi hususani siku 1000 za
kwanza.
Pia
amesema wababa wahusike kwenye malezi ya watoto na jamii ihakikishe
kaya zinauhakika wa chakula kwa kuzalisha vyakula vya kutosha na
kutotumia vyakula vyote kutengeneza pombe.
Amezungumzia
umuhimu wa jamii kutengeneza bustani ndogondogo kuzunguka nyumba,
bustani makasha/viroba kwa ajili ya mboga za majani.Pia kufuga wanyama
wadogo kama kuku na sungura.
Amesema
ukosefu wa virutubisho mwilini husababisha njaa iliyojificha ambayo
huchangia kwa kiwango kikubwa katika kusababisha magonjwa na vifo
hususani kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano na akina mama walio
katika umri wa kuzaa
Kuhusu
mafunzo ya lishe kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini, Msagati
amesema wanatambua nafasi ya vyombo vya habari katika kuelimisha umma.
Msagati
amesema wahariri wa vyombo vya habari ndio wenye jukumu la kupitisha
habari kwenye vyombo vyao na hivyo kukutana kati ya Panita na wahariri
hao kutatoa fursa ya kuelezea umuhimu wa kuzipa kipaumbele habari za
lishe bora.
Mhariri
wa Gazeti la Mtanzania, Bakari Kimwanga na Mgariri wa Jarida la Afya na
Ajira kutoka Gazeti la Mwananchi, Lilian Timbuka wamezungumzia umuhimu
wa mafunzo yaliyotolewa na Panita kuhusu lishe bora na kwamba watatumia
vyombo vyao kuwa mabalozi wa kuhamasisha jamii kuzingatia lishe bora.
Meneja
wa Program wa Jukwaa la Lishe Tanzania(Panita), Jane Msagati akitoa
mada kwenye semina ya wahariri wa vyombo vya habari iliyofanyika leo Dar
es Saalam leo Semina hiyo ilikuwa inangumzia umuhimu wa lishe bora kwa
jamii.
Mwandishi
Mwandamizi wa Mlimani TV, Annuary Mkama akitoa somo kuhusu umuhimu wa
lishe bora kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini.
Wahariri
na waandishi wa habari wakisikiliza mtoa mada katika semina la lishe
bora kutoka kwa Meneja wa Programu wa Panita Jane Msagati(hayupo
pichani).
Mtaalam
wa masuala ya lishe kutoka Jukwaa la Lishe Tanzania(Panita), Deborah
Esam akitoa mada kwa wahariri wa vyombo vya habari kuhusu umuhimu wa
lishe bora kwa jamii.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...