MAAFISA Habari na Mawasiliano katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini wametakiwa kuacha kufungia katika makabati na makabrasha taarifa chanya za utekelezaji wa mikakati, miradi na programu mbalimbali za Serikali na badala yake watangaze mafanikio hayo kwa umma.
Hayo yamesemwa jana (Jumanne Machi 20, 2018) Mkoani Morogoro na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Rodney Thadeus wakati wa ufunguzi wa mafunzo kuhusu mwongozo wa uandishi wa habari za tovuti kupitia Mradi wa Uimarishaji Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani (USAID).
Thadeus alisema Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini, hivyo ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano katika maeneo hayo watangaze mafaniko hayo badala ya kusubiri maswali na hoja mbalimbali za wananchi wakihoji katika kupata uelewa kuhusu miradi hiyo.
“Maafisa Habari, msifungie taarifa katika makabati yenu toeni taarifa kwa Umma, wananchi wanapenda kufahamu nini kinafanywa na Serikali yao hivyo jukumu la Afisa Habari ni kupiga picha kuandaa taarifa na wekeni vielelezo hivyo katika tovuti zenu ili kujibu hoja za wananchi” alisema Thadeus.
Aidha, alisema ni wajibu wa Maafisa Habari na Mawasiliano kuhakikisha kuwa wanaweza taarifa mpya kila wakati ili kuhakikisha kuwa zinakidhi mahitaji ya msingi ya wananchi ambao wamekuwa wakitumia muda mrefu kwa ajili ya kutafuta huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali katika maeneo yao ya kazi.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Rodney Thadeus akizungumza na
Maafisa Habari na Mawasiliano kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya
Morogoro, Manyara, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga yaliyofunguliwa jana
jumanne Machi 20, 2018. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na
Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili
wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).
Mwezeshaji
na Afisa Habari kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI, Nteghenjwa Hosseah
akiwasilisha mada kuhusu mtindo wa uandishi wa habari katika tovuti
kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma,
Kilimanjaro na Tanga yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018.
Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya
Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa
mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada
la Marekani (USAID).
Baadhi
ya washiriki wa mafunzo ya uandishi wa habari za tovuti kutoka katika
Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga
wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mafunzo hayo yaliyofunguliwa jana
Jumanne Machi 20, 2018 Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo ya siku nne
yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa
kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID)
Baadhi
ya washiriki wa mafunzo ya uandishi wa habari za tovuti kutoka katika
Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini wakifuatilia mada mbalimbali
wakati wa mafunzo hayo yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018
Mkoani Morogoro. Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na
Uimarishaji Mifumo ya Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili
wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).
Afisa
Tehama kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro, Alfred
Chali akichangia hoja wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za tovuti
kutoka katika Halmashauri na Mikoa ya Morogoro, Manyara, Dodoma,
Kilimanjaro na Tanga yaliyofunguliwa jana Jumanne Machi 20, 2018.
Mafunzo hayo ya siku nne yamendaliwa na Mradi na Uimarishaji Mifumo ya
Sekta ya Umma (PS3) kwa kushirilkiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa
mna Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia ufadhili wa Shirika la Misaada
la Marekani (USAID).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...