Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
CSHIRIKA la
Reli Nchini (TRC) imeingia mkataba wa ununuzi vichwa vya trein 11 na kampuni ya
Progress Rail Locomotives (PRL) ya Marekani ili kuweza kuongeza idadi ya vichwa
katika shirika hilo
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Masanja Kadogosa amesema kuwa ununuzi wa
vichwa hivyo itafanya shirika kuwa vichwa 47.
Amesema
walikuwa na vichwa 29 ambavyo kwa mahitaji vilikuwa havitoshi lakini kwa sasa
shirika linatakuwa vichwa vya kutosha katika kutoa huduma nzuri kwa wateja wa
Trein.
Amesema kuwa
vichwa vitafanya majaribio katika awamu tatu ambapo ya kwanza ni kuangaliwa na
watalaam katika ubora wake na awamu nyingine kuviwasha na kupakia tani 700 toka
Dar es Salaam pamoja na hatua ya tatu kupakia tani 1200 toka Morogoro hadi Kigoma na Mwanza.
Kadogosa
amesema serikali imeokoa zaidi dola 8,800,000 kwa kila kichwa kutoka dola 3 200,000 kutokana na na
mazungumzo ya kamati.
Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa Meneja wa Kanda wa Nchi za Afrika zilizo Jangwa la Sahara wa Kampuni ya Progress Rail Caterpillar, Barend Hanekom wakibadilishana mikataba mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano
Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa Meneja wa Kanda wa Nchi za Afrika zilizo Jangwa la Sahara wa Kampuni ya Progress Rail Caterpillar, Barend Hanekom wakionesha mikataba kwa waandishi habari mara baada ya kusaini jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...