Na Agness Francis, Globu ya jamii

UONGOZI wa Singida United umekana kufungiwa kwa mchezaji wa timu yao Danny Lyanga kwa kosa la kusaini mikataba timu mbili.

Taarifa zilizoenekana kupitia kwa vyombo mbalimbali vya habari, ikielezea kuwa Lyanga amefungiwa na Shirikisho la Mpira duniani (FIFA) kutokana na kudaiwa kusaini kuzitumikia timu mbili ambazo ni Singida United na Fanja Fc ya Oman.

Hivyo FIFA na kuamua kumfungia mchezaji huyo Danny Lyanga kwa muda wa miezi sita kwa kosa la kusaini mkataba timu mbili. Ambapo inasemekana kuwa alisaini mkataba na Singida United wakati wa dirisha dogo akiwa bado ana mkataba wa miaka miwili na klabu ya Fanja FC ya Oman.

Hata hivyo uongozi wa Singinda United umekananusha uvumi huo na kusema si kweli.Umefafanua Lyanga ni mchezaji wao halali wamemsajili kutoka Fanja Fc ya Oman na kufanya makubaliano ya mkataba ambao ulionyesha kuwa mchezaji huo ameshamalizana na kikosi hicho na kuwa huru kununuliwa na Timu nyingine.

Imeelezwamchezaji hiyo hajafungiwa na FIFA miezi 6 kama inavyodaiwa. Kilichotokea mpaka kupelekea uvumi huo kusambaa katika vyombo mbalimbali vya habari ni kuchelewa kupata kibali cha kuchezea nje ya Nchi (ITC) kutoka Fanya Fc. 

"Kilichotokea ni kwamba ITC ya Danny Lyanga iljchelewa kuja kutokana na dirisha la usajili kufungwa, hivyo FIFA walituandikia barua sisi pamoja na TFF kwamba ITC ya Lyanga itakamiIika hadi hapo dirisha kubwa la usajiri litakapofunguliwa hapa Tanzania kuanzia Julai 2018.

"Hivyo basi Danny Lyanga hajafungiwa na hivi tunategemea kumtumia kwenye Michuano ambayo klabu yetu itakwenda kushiriki nje ya Nchi"amesema msemaji wa uongozi huo.Uongozi umesema "Tunaomba vyombo vya habari kutumia taarifa rasmi kutoka vyanzo rasmi kwa ajili ya maslai ya Mpira wa miguu hapa nchini".

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...