Na Bashir Yakub.

Unaweza kuwa wewe, ndugu yako,rafiki au  jamaa yako ameunganishwa katika kesi ya mauaji. Aghalabu, daktari anasubiriwa kutoa ushahidi mahakamani kuhusu sababu za kifo cha marehemu.

 Na ni ushahidi huo wa daktari utakaokuondoa katika kesi  hiyo ya mauaji au utakuingiza katika kesi hiyo na hivyo kutiwa hatiani na kuadhibiwa.

Lakini sio daktari tu bali wenye kesi wote ambao ushahidi wake unahitaji mtaalam(expert) kuthibitisha mfano mkemia, mtaalam wa muandiko na sahihi, mtaalam wa biashara , mtaalam wa DNA  nk.

1.USHAHIDI WA DAKTARI.

Kifungu chac 47 cha Sheria ya Ushahidi kinaruhusu kutumika na kukubalika kwa ushahidi wa mtaalam( expert). Mtaalam ni pamoja na daktari.

2. MAMBO  6  MUHIMU UNAYOTAKIWA KUJUA.
A ).  Kabla daktari au mtaalam mwingine yoyote hajaanza kutoa ushahidi wake ni ni muhimu sana athibitishe kwa ushahidi kuwa yeye ni mtaalam kweli (expert) kwa hicho anachotaka kutolea ushahidi. Usikubali akaanza  kueleza kabla ya kuthibitisha utaalam.Mtake athibitishe hilo kwanza.

Utaalam unathibitishwa kwa taaluma(professional). Kama ni daktari na mtaalam wa eneo fulani la tiba ,mfano mifupa, moyo, nk, aoneshe cheti cha taaluma katika eneo hilo. Halikadhalika kwa wataalam wengine nao wanatakiwa kufanya hivyo. Kama hawezi kuthibitisha hilo basi hiyo ni faida kwako kwakuwa ushahidi wake ni wa kutia shaka.

Na hapo haijalishi mtaalamu(expert) huyo ameletwa na nani. Awe ameletwa na polisi, PCCB, au idara nyingine yoyote. Msimamo huu ulitolewa na mahakama  katika kesi ya MUHAMMED AHMED V 

REPUBLIC(1957)E.A. C.A 523.
B ). Daktari au shahidi yoyote mtaalam, asiwe tu mtaalam wa vyeti, bali awe mwenye ujuzi wa uzoefu wa kazi husika. Kwa mfano, daktari au mtaalam ambaye amemaliza chuo, ana cheti lakini hajaajiriwa wala kuwahi kuifanyia kazi taaluma yake popote hawezi kuitwa mtaalam mwenye uwezo(competence) wa kutoa ushahidi wa kitaalam.
                 
   KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...