Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii

WANAFUNZI wa kike 110  waliotekwa February 19 katika shule ya bweni Dapchi nchini Nigeria  wamerejeshwa nyumbani kutoka kwenye mikono ya waasi.

Waziri wa habari nchini humo Alhaj Lai Mohammed ameeleza kuwa wanafunzi 101 kati ya 110 wamerejeshwa salama na hiyo ni baada ya jeshi kuweka juhudi ili kunusuru maisha ya watoto hao.

Licha ya Wizara kutothibitisha inasemekana wasichana watano wamefariki dunia na hiyo ni kutokana na maeleza ya Aisha Kachalla Bukar (14) mmoja wa manusura hao aliyoyatoa kwa baba yake.

 Pia inasadikika kuwa mmoja wa wanafunzi hao(mkristo) bado anaendelea kushikiliwa na waasi hao baada ya kukataa kuslimu.Rais wa nchi hiyo Muhammadu Buhari ameeleza kuwa janga la utekaji ni la kitaifa na ametoa pole kwa waathirika wote.

Ifahamike kuwa mwaka 2014 wanafunzi 300 walitekwa huko Chibok na hadi sasa wanafunzi 100 bado hawajapatikana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...