Na Genofeva Matemu – WHUSM
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amemtaka Msanii wa muziki wa bongo fleva Roma Mkatoliki kujisajili BASATA ili aweze kuondolewa kwenye kifungo chake cha kutokufanya shughuli za sanaa kwa miezi sita alichofungiwa mwanzoni mwa mwezi machi mwaka huu.
Hayo ameyasema wakati wa kikao na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam baada ya kikao na wasanii wa mziki Roma Mkatoliki na Pretty Kind ambapo Wizara ilimtaka msanii Roma kubadilisha wimbo wake wa kibamia na kujisajili BASATA ili aweze kuondolewa katika kifungo hicho ambapo msanii huyo alitangaza kuufuta wimbo huo na kuahidi kujisajili BASATA ili aweze kuendelea na mziki.
“Kwa kuwa msanii Roma Mkatoliki ameamua kuufuta kabisa wimbo wa kibamia na kuvitaka vyombo vya habari kutokuucheza tena wimbo huo Wizara inamfungulia kifungo chake mara tu baada ya kujisajili BASATA atakuwa huru kuendelea na kazi zake za sanaa” amesema Mhe. Mwakyembe
Aidha Naibu Waziri Shonza amesema kuwa Msanii Suzan Michael (Pretty Kind) ametambua kosa alilolifanya na kukiri kosa hilo kwa kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuandika barua ya kuomba msamaa na kujisajili BASATA kuwa msanii halali hivyo Wizara kwa kushirikiana na BASATA imeridhia kumfungulia adhabu aliyopewa ya miezi sita ambayo kimsingi ilitakiwa kuisha tarehe moja julai mwaka huu. 
“Kuanzia sasa msanii Pretty Kind yupo huru kuendelea na kazi zake za sanaa kutokana na yeye kutimiza matakwa aliyoagizwa kuyafanya na kuahidi kuwa balozi mwema wa masuala ya maadili kwa wasanii wenzake” amesema Mhe. Shonza.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kufanya kikao na wasanii wa mziki Roma Mkatoliki na Pretty Kind jana jijini Dar es Salaam. Pembeni kwa waziri ni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza
 Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao na waandishi wa habari baada ya kufanya mazungumzo na wasanii Roma Mkatoliki na Pretty Kind jana Jijini Dar es Salaam. Katikati ni mwakilishi kutoka Bodi ya Filamu Bw. Benson Mkenda na kushoto ni msanii wa mziki Pretty Kind
 Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akiwaonyesha waandishi wa habari nakala ya cheti cha usajili cha msanii Pretty Kind kutoka BaASATA wakati wa kikao na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
 Msanii wa mziki wa bongo fleva Roma Mkatoliki (kulia) akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam baada ya kufanya kikao na Waziri pamoja na Naibu Waziri ambapo alitangaza kuufuta na kuviomba vyombo vya habari kutoucheza tena wimbo wake wa kibamia. Kushoto ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe katika picha ya pamoja na Msanii Roma Mkatoliki (wapili kushoto) na msanii Pretty Kind (kulia) baada ya kuzungumza nao na kurekebisha tofauti zilizopelekea kufungiwa kwa wasanii hao jana Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza 
Picha na: Genofeva Matemu - WHUSM

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...