WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Mwigulu Nchemba anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika Aprili Mosi mwaka huu katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo, Alex Msama amesema kuwa Nchemba amethibitisha kuwa mgeni rasmi kwenye tamasha hilo.

Msama ameongeza kuwa awali mgeni rasmi alikuwa awe Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samiah Suluhu lakini imeshindikana kutokana na kukabiliwa na majukumu mengine ya kikazi na hivyo Waziri Mwigulu atamwakilisha katika uzinduzi wa tamasha hilo.

Mbali na Mwigulu, viongozi wengine wanaotarajiwa kuhudhuria hafla hiyo ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maendeleo na Makazi, Angelina Mabula, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi.

Aidha, Msama amesema kwamba katika tamasha hilo kunatarajiwa kuwakutanisha zaidi ya waimbaji wa kitaifa na kimataifa na akawataja baadhi ya waimbaji ambao tayari wamethibitisha kuhudhuria kuwa ni, Rose Mhando, ambaye atazindua albamu yake mpya ya ‘Usivunjike Moyo’, Angel Benard, Bonny Mwaitege, Jesca Honore, Christina Shusho, Christopher Muhangila, Upendo Nkone na wengine kibao.

“Niwaambie ndugu waandishi wa habari, maandalizi yanaenda vizuri kwani tumejipanga vyema kuhakikisha wananchi watakaofika siku hiyo wanapata burudani ya kutosha na kulishwa neno la Mungu kupitia ujumbe wa nyimbo za waimbaji na ulinzi wa kutosha utakuwepo kwani tayari jeshi la polisi litakuwepo kuhakikisha amani na utulivu upo na hivyo nawaomba wakazi wa maeneo hayo wajitokeze kwa wingi,” amesema.

Amebainisha kuwa viingilio siku hiyo kwa wakazi wa Mwanza na maeneo mengine yanayozunguka eneo hilo kwamba vitakuwa ni Shilingi 5,000 kwa wakubwa na shilingi 2,000, kwa watoto huku kwa Mkoa wa Simiyu Aprili 2 mwaka huu, wakubwa wataingia kwa shilingi 3,000 na watoto 2,000.
Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama akitoa ufafanuzi juu ya ujio wa mgeni rsmi ambaye ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu ambaye atawakilishwa na  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Mwigulu Nchemba. Kushoto ni Mratibu wa Tamasha hilo, Jimmy Charles (kushoto). 

Baadhi ya Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mwandaaji wa tamasha la Pasaka kanda ya Ziwa,Alex Msama alipokuwa akielezea kukamilika kwa maandalizi ya tamasha hilo sambamba na mambo mbengine mbalimbali

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...