Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema ni muhimu kuwekwa mikakati ya kukabiliana na uharibifu unaoendelea katika vyanzo mbalimbali vya maji na misitu nchini.

Mhandisi Kamwele amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Maji Duniani na kwa Tanzania lengo lake ni kuangalia uwezekano wa kuwapatia maji safi na salama kwa watanzania wote.

Aidha ameeleza mkakati wa kuvuna maji ya mvua ili kupata maji shuleni kupitia matanki na visima vya kujenga ambapo anaamini itasaidia kuondoa changamoto ya uhaba wa maji shuleni.

Pia ameeleza mafanikio katika suala la maji na majengo katika shule za Kirumba na Isenyi jijini Mwanza pia katika ujenzi wa vyoo na vyumba kwa wanafunzi wa kike.

Ameshukuru Benki ya dunia, Serikali ya Korea  na Mpango wa maendeleo Ufaransa kwa ushirikiano wao katika suala la maji na utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji ni lazima.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza wakati wa kufungua Mkutano wadau wa maji uliandaliwa na benki ya Dunia nchini uliokwenda kwa jina la 'TANZANIA WASH POVERTY DIAGNOSTIC' uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam.
 Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Malawi na Burundi, Bella Bird akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Maji na Umwagiliaji kufungua mkutano huo muhimu kwa ajili ya maji Tanzania.
 Mwasilishaji wa mada juu ya kupinga umaskini na uhaba wa maji  Mchumi wa Benki ya Dunia, George Joseph akizungumza na wadau wa maji waliofika katika mkutano huo.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini(TUDARCO), Prof.  Uswege  Minga  akizungumzia na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa utunzaji wa maji na na mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na baadae.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...