Na Pamela Mollel,Arusha

UKATA wa fedha katika uwekezaji na kukuza biashara ya utalii mkoani hapa umepata tiba baada ya Commerial Bank of Africa, kusema itashirikiana na wafanyabiashara kuwapa mikopo hadi kufikia dola za Marekani milioni 50 kwa atakayetaka.

Mkuu wa Idara ya Masoko wa benki hiyo, Julius Konyani, alisema wafanyabiashara 500 katika sekta ya utalii mkoani hapa kila mmoja anaweza kukopeshwa dola za Marekani milioni 50.Alisema hayo katika ya katika chakula cha jioni walichoandaa kwa ajili ya kubadilishana nao mawazo na wateja wao.

“Mteja mmoja anaweza kukopeshwa dola za Marekani milioni 50, tunaweza kuwakopesha wateja 500 hapa Arusha kila mmoja kiasi hicho cha mkopo hapa,” alisema.Alisema benki yake imefanya utafiti kwa mikoa mbalimbali kuangalia fursa zilizopo kama vile kilimo na utalii, na hivyo, imejipanga kuwawezesha wateja hao kukopa kiasi wanachohitaji ili kuendeleza na kukuza uwekezaji katika mkoa yao.

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Benki ya Commerial Bank of Africa (CBA) Tanzania, Gift Shoko akizungumza na wadau wa benki hiyo katika hafla fupi ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo katika hoteli ya Mt. Meru jijini Arusha, huku akiwajulisha hatua mbalimbali za kibenki zilizoboreshwa kwa wateja wao (Habari picha na Pamela Mollel Arusha)
Wadau wa benki ya Commerial Bank of Africa,CBA wakiwa katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Arusha kwa lengo la kuwajulisha hatua mbalimbali walizozifikia huku wateja wao wakipata wasaa wa kueleza changamoto zinazowakabili.
Mkurugenzi Mkuu Mendaji wa Be Gift Shoko kushoto akizungumza na mmoja wa wadau wa benki hiyo jijini Arusha 
Mkuu wa Idara ya Masoko wa benki ya CBA, Julius Konyani akizungumza katika hafla ya chakula cha jioni na wadau wa benki hiyo jijini Arusha kwa lengo la kuwajulisha hatua mbalimbali walizozifikia huku wateja wao wakipata wasaa wa kueleza changamoto zinazowakabili.

Wadau wa benki hiyo wakiwa katika hafla ya chakula cha jioni jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...