Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amekutana na wakazi wa kijiji cha Nyambui kilichopo katika kata ya Tinde halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kutatua mgogoro wa eneo la ujenzi wa mradi wa mnada utakaotumika badala ya ule uliopo hivi sasa. 

Mkuu huyo wa wilaya amefika katika kijiji hicho kutatua mgogoro huo leo Ijumaa Aprili 20,2018 akiwa ameambatana na maafisa mbalimbali wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga. 

Akizungumza wakati wa kikao hicho,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro aliiagiza halmashauri kupima eneo hilo na kuboresha miundo mbinu ya mnada mpya huku akisisitiza wananchi wazawa kupewa kipaumbele katika maeneo ya biashara. 

“Niiagize halmashauri kuwa sasa tunapokwenda kuuboresha huu mnada,ni lazima kwanza tuwape kipaumbele wazawa wa eneo hili kwa sababu walikuwepo tangu mwanzoni,wakaiachia serikali kwa ajili ya maendeleo, tukishamaliza basi maeneo yanayobaki tutawapa wageni watakaokuja kufanya biashara hapa bahati nzuri majina yenu tunayo hivyo kazi itakuwa rahisi’,alieleza Matiro. 

“Tunataka tufanye mnada hapa na mnada huu unatupa pesa kama halmashauri,hivyo miundo mbinu kama choo,maji,ofisi lazima viwekwe kwenye utaratibu kabla mnada huu mpya haujaanza na tutakuja kukagua ili tuone kama yale tuliyoagiza yanafanyika? kazi ya kwanza inayotakiwa hapa ni kupima eneo na kuweka mpango kazi”,aliongeza. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nyambui kata ya Tinde halmashauri ya wilaya ya Shinyanga leo Aprili 20,2018 - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wakazi wa Nyambui na kuwataka kushirikiana na serikali katika miradi ya maendeleo - Kulia ni mwenyekiti wa kijiji cha Nyambui Richard Mpanga ,Kushoto ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Ngasa Mboje
Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Thomas Tukay akifafanua jambo wakati wa kikao hicho
Katibu tawala wilaya ya Shinyanga, Boniface Chambi akizungumza katika kikao hicho .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...