Wagonjwa 467 wenye matatizo ya moyo wamebainishwa na kupatiwa huduma ya ushauri na matibabu kutoka kwa madaktari bingwa waliotoa huduma kwenye kambi maalumu ya siku 4 katika hospitali ya Vwawa-Mbozi Mkoani Songwe.

Timu ya Madaktari Bingwa na wauguzi 5 wameeleza kuwa wagonjwa 18 kati ya hao waliowahudumia wamepewa rufaa ya kufika hospitali za Rufaa kwa ajili ya matibabu Zaidi.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo George Lyego Longopa Kutoka Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete amesema wameanza matibabu siku ya Jumanne na kila Daktari amekuwa akiona zaidi ya wagonjwa 60 kutokana na hamasa ya wagonjwa waliojitokeza kupata matibabu ya magonjwa ya moyo.

 “Tumeona wagonjwa wengi na tumeamini kuwa Songwe tatizo la Magonjwa ya moyo bado ni kubwa, wagonjwa wengi wamekutwa na matatizo ya shinikizo la damu, moyo kushindwa kufanya kazi vizuri pamoja na matatizo ya mishipa ya damu kuziba”, amesema Dkt Longopa.

Afisa Muuguzi Kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Flora Kasembe ameeleza kuwa mtindo wa maisha ya wananchi wa Songwe unaweza kuwa ni chanzo cha magonjwa ya moyo hasa kutokana na uwepo vyakula vingi lakini wananchi hawali mlo kamili.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo George Lyego Longopa Kutoka Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Jakaya Kikwete akichukua maelezo ya mgonjwa wa moyo katika hospitali ya Vwawa-Mbozi.
 Afisa Muuguzi Kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Flora Kasembe akimpima shiniko la damu mwandishi wa habari Manuel Kaminyoge katika hospitali ya Vwawa-Mbozi,
 Baadhi ya wagonjwa wakisoma kipeperushi kinachoeleza masuala ya lishe wakati wakisubiri kupata huduma ya madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika hospitali ya Vwawa-Mbozi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...