Hivi ndivyo hali ilivyokuwa katika eneo la Jangwani jijini Dar es salaam, baada ya Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mengi hapa nchini, hali iliyofanya Mto Msimbazi kufurika maji na kupelekea sehemu ya eneo hilo katika barabara ya Morogoro kufungwa kwa muda. hali hiyo pia ilisababisha kituo cha mabasi yaeneondayo haraka (UDA RT) kufungwa na mabasi yote kusitisha safari zake za kuelekea maeneo ya katikati ya mji. Kwa mujimu wa Mamlaka ya hali ya hewa nchini, hali hii ya mvua inatazamiwa kuendelea hadi hapo Aprili 19, 2018, hivyo Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhali ya mvua hiyo ambayo inaweza kuleta madhara.
 Maji yakiwa yameenea kisa sehemu ya eneo la Jangwani.
 Mmoja wa wakazi wa maeneo ya jirani na Jangwani akisaka chochote kwenye maji hayo, bila kujali usalama wake.
 Nyumba zilizo kando ya eneo la Jangwani zikionekana kujaa maji.
 Eneo la Jangwani linavyoonekana kutokea upande wa Mapipa, Magomeni.
 Maji ni mengi sana.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...