Editha Karlo,Blog ya jamii Kigoma

MKUU wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga ameupokea Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2018 leo kutoka kwa Mkuu wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu katika kijiji cha Nyamtukuza Eilayani Kakonko ambapo mwenye huo utatembela miradi 50 yenye thamani ya Sh.bilioni 12.97.

Mwenge huo utakimbizwa katika halmashauri zote nane za Mkoa wa Kigoma na kati ya miradi hiyo miradi 24 itazinduliwa, miradi 11 itafunguliwa, miradi 11 itawekewa mawe ya msingi na miradi 2 itakaguliwa. 

Pia miradi 2 itakuwa ya uwezesho wa vikundi vya wajasiriamali vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Mwenge wa mwaka huu umebeba ujumbe wa kauli mbiu"Elimu ni ufungo wa maisha wekeza sasa kwa maedeleo ya Taifa letu".

Kiongozi wa mbio za Mwenge mwaka huu kitaifa ni Charles Kabeho(Dar es salaam)akishirikiana na Issa Abasi(Kusini Pemba)Agusta Safari(Geita)Ipyana Mlilo(Tanga)Dominick Njunwa(Kigoma)na Riziki Hassa(kusini Unguja).

Aprili 24 mwaka huu Mwenge huo utahitimisha mbio zake mkoani humo na kukabidhiwa mkoani Tabora kwa ajili ya kuendelea na mbio zake.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga akisoma taarifa ya Mkoa ya miradi ya mwenge kwa kiongozi mwenge 2018 Charles Kabeho.
Mkuu wa Mkoa wa kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga akimkabidhi mwenge wa uhuru 2018 Mkuu wa Wilaya ya Kakonko kanali Hosea Ndagalu kwa ajili ya kuukimbiza katika Wilaya yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...