Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
HATUNAYE TENA! Hiyo ndio kauli unayoweza kuielezea baada ya
kuwepo kwa taarifa za kufariki dunia kwa video queen hot zaidi
nchini na muigizaji wa filamu Agnes Gerald maarufu kama Agnes Masogange.
Ni ngumu kuamini kama Masogange amefariki dunia lakini huo
ndio ukweli.Najua itakuchua dakika kadhaa kutafakari kifo cha
binti huyo mwenye urembo wake na aliyejaaliwa kuwa na mvuto
kwa mwenye kuona.
Taarifa kuhusu kifo cha Masogange zinaeleza amefariki dunia leo
Aprili 20 , mwaka huu katika Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo
Mwenge Dar es Salaam. Masogange amefariki dunia akiwa bado
binti mwenye umri mdogo tu hasa kwa kuzingatia amezaliwa
mwaka 1989.
Hata hivyo haijafahamika sababu za kifo chake zaidi ya kuelezwa tu amefariki baada ya kuugua muda mfupi na kukimbizwa hospitalini hapo ingawa wapo wanaosema kifo chake kimesababishwa na shinikizo la damu.
Aidha Michuzi Blog imeshuhudia Mwili wa Marehemu Agness Masogange ukiondolewa kituo cha Afya cha Dkt Ngoma na kupelekwa kuhifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili jioni hii.
Kifo chake ni pigo kwa Watanzaia walio wengi na hasa mashabiki
wa muziki wa kizazi kipya kwani pamoja na kufanya shughuli zake
binafsi lakini alipata umaarufu zaidi baada ya kuanza kutumiwa na
wasanii maarufu katika nyimbo zao.
Ni hivi karibuni tu Masogange alitikisa vyombo vya habari nchini
baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumhukumu kwenda
jela miaka miwili au kulipa faini ya Sh.milioni 1.5 baada ya kutiwa
hatiani kwa makosa mawili la kutumia dawa za kulevya aina ya
heroine na pili kutumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.
Hata hivyo Masogange katika kipindi chote cha kesi hiyo ya dawa
za kulevya hakuwahi kukanusha na baada ya kutolewa hukumu
alilipa faini ya Sh.milioni 1.5 na akatangaza kuwa a furaha ya aina
yake kwani alikuwa anabanwa na hata alipotaka kusafiri ilikuwa
lazima apate kibali.
Hatimaye pamoja na Watanzania kumpenda zaidi Muumba wa
Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo amemuita.
Bwana ametoa na
Bwana ametwaa.
Kwake sote tutarejea.
Amina
HATUNAYE TENA! Hiyo ndio kauli unayoweza kuielezea baada ya
kuwepo kwa taarifa za kufariki dunia kwa video queen hot zaidi
nchini na muigizaji wa filamu Agnes Gerald maarufu kama Agnes Masogange.
Ni ngumu kuamini kama Masogange amefariki dunia lakini huo
ndio ukweli.Najua itakuchua dakika kadhaa kutafakari kifo cha
binti huyo mwenye urembo wake na aliyejaaliwa kuwa na mvuto
kwa mwenye kuona.
Taarifa kuhusu kifo cha Masogange zinaeleza amefariki dunia leo
Aprili 20 , mwaka huu katika Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo
Mwenge Dar es Salaam. Masogange amefariki dunia akiwa bado
binti mwenye umri mdogo tu hasa kwa kuzingatia amezaliwa
mwaka 1989.
Hata hivyo haijafahamika sababu za kifo chake zaidi ya kuelezwa tu amefariki baada ya kuugua muda mfupi na kukimbizwa hospitalini hapo ingawa wapo wanaosema kifo chake kimesababishwa na shinikizo la damu.
Aidha Michuzi Blog imeshuhudia Mwili wa Marehemu Agness Masogange ukiondolewa kituo cha Afya cha Dkt Ngoma na kupelekwa kuhifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili jioni hii.
Kifo chake ni pigo kwa Watanzaia walio wengi na hasa mashabiki
wa muziki wa kizazi kipya kwani pamoja na kufanya shughuli zake
binafsi lakini alipata umaarufu zaidi baada ya kuanza kutumiwa na
wasanii maarufu katika nyimbo zao.
Ni hivi karibuni tu Masogange alitikisa vyombo vya habari nchini
baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumhukumu kwenda
jela miaka miwili au kulipa faini ya Sh.milioni 1.5 baada ya kutiwa
hatiani kwa makosa mawili la kutumia dawa za kulevya aina ya
heroine na pili kutumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.
Hata hivyo Masogange katika kipindi chote cha kesi hiyo ya dawa
za kulevya hakuwahi kukanusha na baada ya kutolewa hukumu
alilipa faini ya Sh.milioni 1.5 na akatangaza kuwa a furaha ya aina
yake kwani alikuwa anabanwa na hata alipotaka kusafiri ilikuwa
lazima apate kibali.
Hatimaye pamoja na Watanzania kumpenda zaidi Muumba wa
Mbingu na Ardhi na vyote vilivyomo amemuita.
Bwana ametoa na
Bwana ametwaa.
Kwake sote tutarejea.
Amina
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...