Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii
IMEELEZWA kuwa watu pekee  wanaoweza kumaliza migogoro ya ardhi nchini ni pande mbili zinazogomnana, na wataalamu wakienda ni kwa ajili tu kuweka mipaka ya kisheria ili mgogoro usijirudie tena.

Mwenyekiti wa Halmashaui ya Wilaya ya Morogoro Kibena Kimu amesema hayo leo wakati wa ufunguzi wa mdahalo wa  haki za ardhi wilayani ya Morogoro uliondaliwa na Shirika la mradi la PELUM Tanzania unaofanyika kwa siku mbili na kushirikisha vijiji vitano vya Mikese Lubungo, Newland na Mfumbwe  vya wilayani humo.

Amesema huwezi kumaliza siku bila kupata taarifa ya mgogoro wa ardhi kutoka kwa wakulima na wafugaji au kijiji na kijiji, kuhusu mipaka kuwa kila mmoja akidai kaingiliwa na mwenzake, mara  huyu kaniingilia na huyu naye akidai kaingiliwa, lakini hata wataalamu wakienda na GPS hawawezi kutatua mgogoro huo.

"Mara  nyingi wataalamu wakifika kila mmoja anaonesha mpaka wake, mwingine anasema mpaka wa kimila ni huu hapa hali inayofanya kutopatikana kwa ufumbuzi.

  Mwenyekiti wa Halimashauri ya Wilaya ya Morogoro, Kibena Kimu ambaye ni mgeni rasmi wa kongamano la haki za ardhi wilaya ya Morogoro akizungumza na wadau wa ardhi kuashiria ufunguzi wa kongamano hilo linalofanyika mjini Morogoro humo kwa siku mbili.

Mada kubwa katika kongamano hilo ni usimamizi sahihi wa mpango wa matumizi ya ardhi na uundwaji wa vyombo vya utatuzi wa migogoro ya ardhi jinsi vinavyosaidia kupunguza migogoro hiyo vijijini.
 Meneja Miradi wa PELUM Tanzania, Rehema Fidelisi akizungimza juu kuwapatia hati miliki za kimila wanakijiji kutoka vijiji vya Mikese, Lubungo, Newland na Mfumbwe vilivyopo Wilayani Morogoro.
 Afisa mradi wa  mradi wa ushirika wananchi katika kusimamia sekta ya Kilimo (Sego), Anna Marwa akielezea na kuchambua mafanikio na Changamoto za utekelezaji wa mradi huo, katika mdahalo wa haki za ardhi wilaya ya Morogoro unaofanyika Wilayani humo kwa siku mbili.
Mhadhiri kutoka chuo cha Kilimo Sokoine ambaye ni mshereheshaji  Emmanuel Malisa akizungumza katika Mdahalo wa haki za ardhi wilayani Morogoro.
Afisa Ardhi wa Maliasili Wilaya ya Morogoro, Wahida Beleko, akizungumza katika Mdahalo wa haki za ardhi wilayani humo unaofanyika kwa siku mbili mfululizo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...