Qatar Airways yapeleka waandishi kutoka vituo mbalimbali vya
habari na utangazaji vya Africa kwa
ajili ya matembezi mjini Doha. Katika matembezi hayo wanahabari walipata fursa
ya kutembelea maeneo mbalimbali kama Makumbusho ya Sanaa ya kiislamu (museum of
Islamic art) haya ni makumbusho yaliyopo katika mji mkuu wa Qatar, Doha. Pia
walitembelea Kijiji cha kitamaduni cha Katara, Katara ni kijiji kitamaduni huko
Doha, Qatar.
Iko katika pwani ya mashariki kati ya West Bay na Lulu ambayo Ilifunguliwa
mnamo Oktoba 2010. Walitembelea The Grand Mosque, Msikiti wa Kitaifa Qatar. Huu
ni mojawapo ya misikiti mikubwa ya kihistoria nchini Qatar, Msikiti huu uko
katika wilaya ya Jubailat Doha. Wanahabari hao pia walipata nafasi ya
kutembelea maeneo kama Souq waqif, Falcon souq, na Gold souq ambapo waliweza
kujionea vitu vingi kama mapambo na vito vya thamani vilivyotengenezwa kwa
dhahabu na madini ya aina mbalimbali.
Katika ziara yao mjini Doha waandishi wa habari walitembelea
Qatar foundation, Al Shaqab sehemu ambayo hutumika kuwapa mafunzo farasi katika
jamii za kiarabu, the Pearl na Khalifa International Stadium; ambayo
inajulikana kama Uwanja wa Taifa, ni uwanja unaotumika kwa shughuli mbalimbali
huko Qatar ambao pia ni kama sehemu ya eneo la Doha Sports City, ambalo
linajumuisha Aspire Academy, Kituo cha Hamad Aquatic, na Aspire Tower park.
Uwanja ulipewa jina hilo baada ya Khalifa bin Hamad Al Thani, ambaye zamani alikuwa
kiongozi wa dini ya kiislamu (Emir) nchini Qatar. Mbali na maeneo hayo
wanahabari walitembelea Regency sealine camp, Desert Safari, pia kituo cha
utangazaji cha Al Jazeera.
Qatar Airways ina Zaidi ya miaka 20 katika kutoa huduma za
anga, Ni shirika la ndege ambalo limejishindia tuzo mbalimbali ambapo kwa mwaka
2017 Qatar airways ilipata tuzo nyingi Zaidi ya tano na mwaka huu imeshinda tuzo mbalimbali zikiwemo Crystal
cabin award, Skytrax world airport award 2018, 2018 TripAdvisor travelers’
choice awards na Apex passenger choice award 2018. Qatar Airways imeshinda tuzo
za Skytrax airline of the year mara nne (4) mfululizo katika miaka ya 2011,
2012, 2015 na 2017.
“QATAR
AIRWAYS, GOING PLACES TOGETHER.”
Wanahabari kutoka Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja walipokwenda kutembelea Makumbusho ya sanaa ya kiislamu mjini Doha.
Waandishi na wadau wa habari wakiwa wamepumzika baada ya kuwasili Hamad International Airport mjini Doha, Qatar.
Waandishi na wadau wa habari kutoka nchi mbalimbali za Africa i.e Tanzania, Uganda wakiwa katika picha ya pamoja walipokuwa Doha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...