Baadhi ya wanafunzi wa kike wa Shule za Msingi na Sekondari wakiwa katika maandamano ya kuunga mkono chanjo ya kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kikazi iliyozinduliwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri akitoa maelezo ya awali kuhusu chanjo ya kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wa miaka 14 mkoani Tabora iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana.
Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Queen Mlozi akitoa maelezo ya awali wakati wa uzinduzi chanjo kwa watoto wa kike wa miaka 14 ya kuwakinga na saratani ya mlango wa kizazi jana mkoani humo.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Dkt Gunini Kamba akitoa maelezo ya awali kuhusu chanjo ya kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wa miaka 14 mkoani Tabora iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri(KUSHOTO) akitoa maelezo ya awali kuhusu chanjo ya kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wa miaka 14 mkoani Tabora iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana.Wengine ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt Ginini Kamba (wa pili kushoto) , Katibu wa CCM Mkoa Janeth Kayanda(wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Queen Mlozi(kulia)
Baadhi ya wanafunzi wa kike wa Shule za Msingi na Sekondari wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (hayupo katika picha) jana wakati wa hotuba ya uzinduzi wa chanjo dhidi ya saratani ya mlango wa kikazazi kwa wasichina wa umri wa miaka 14.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...