Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari (TPA) imeadhimisha miaka 13 tangu kuanzishwa huku ikijivunia mafanikio ya kuongezeka kwa biashara kuanzia mwaka 2011.

Pia mapato yamekuwa yakiendelea kupanda na kuanzia Julai mwaka 2017 hadi mwaka 2018 shehena iliyokuwa ikiingia ilianza kupanda na meli zinazoingia kufikia takriban 3000 kwa mwezi.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa TPA wakati akielezea Wiki ya Mamlaka hiyo iliyoanza jana na kilele chake kufikiwa Jumapili.Ambapo watatumia maadhimiaho hayo kueleza walikotoka tangu April 2005, walipo na wanakotarajia kwenda kwa ajili ya kuboresha zaidi huduma kwa biashara. 

Amesema TPA imekuwa ikiendelea kuboresha utoaji wa huduma na kuongeza masoko huku wakikusanya Sh.bilioni 420 kwa kipindi cha miezi sita iliyopita."Mamlaka hiyo, inalenga kuboresha zaidi huduma zake, kwa kuandaa mazingira ya serikali kupata mapato yake kwa kuwa kati ya asilimia 45 hadi kufikia 55 ya kodi inayokusanywa na Mamlaka ya Mapato, hupatikana TPA," amesema.

Kakoko amesema wanatarajia kutekeleza mradi ya ujenzi wa bandari kavu katika baadhi ya mikoa ikiwemo Kigoma, Arusha, Mbeya na hata Mwanza wanalenga kuwapa unafuu wateja wao kutoka nje ya nchi wanaokuwa wakifuatilia bidhaa katika Mamlaka hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Profesa Ignas Rubaratuka akizungumza kuhusiana na maadhimisho ya miaka 13 ya Mamlaka usimamizi wa bandari yaliyoanza leo , jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Mhandisi Deosdidit Kakoko akizungumza na waandishi kuhusiana na mafanikio ya kuanzishwa kwa mamlaka ya usimamizi wa bandari, leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Fransisca Muindi akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na huduma watazozitoa katika maadhimisho ya miaka 13 ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari, leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...