WAKATI maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani kwa nchini Tanzania yaliyoandaliwa na shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) yakitaraji kufanyika mkoani Iringa kitaifa mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amesema mkoa wa Iringa kuwa mwenyeji wa mei mosi ni heshima kubwa katika Taifa .
Akizungumza na wanahabari leo ofisini kwake kuhusiana na maandalizi ya Mei Mosi Kitaifa alisema kuwa mkoa wa Iringa umeteuliwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo ambapo mgeni rasmi atakuwa ni Rais Dkt John Magufuli .
Alisema kuwa katika maadhimisho hayo ya Mei Mosi kitaifa kauli mbiu ni Kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kulenge kuboresha mafao ya wafanyakazi na kuwa kupitia maadhimisho hayo wakazi wa mkoa wa Iringa na wafanyabiashara watapata fursa kubwa ya kujitangaza pamoja na kuonyesha shughuli zao.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza |
Rais wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Tumaini Vyamhokya katikati akiongoza kuimba wimbo wa wafanyakazi wakati wa kikao na wanahabari mjini Iringa .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...