Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
UAMUZI wa kesi inayowakabili viongozi 9 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) akiwemo Mwenyekiti wao Freeman Mbowe ya kufanya maandamano/mkusanyiko usio halali unatarajiwa kutolewa Mei 15 mwaka huu kama iende Mahakama Kuu au laa.
Hatua hiyo inatokana na mvutano wa hoja za kisheria zilizotolewa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Wakili wa utetezi, Peter Kibatala kisha kujibiwa leo na Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri.
Hata hivyo majibu yake Wakili Nchimbi ameiomba Mahakama hiyo kutupilia mbali hoja za utetezi zilizotolewa na Kibatala kwa madai zitasababisha ucheleweshaji wa shauri hilo.Nchimbi amefafanua kwa kudai mazingira ya mwenendo wa kesi hiyo toka ilipoanza hadi leo hakuna swali lolote la msingi lililoibuliwa na upande wa utetezi ambalo linajikita na uvunjifu ama ukiukwaji wa haki ya kikatiba.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...