SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), limeanza kutoa mafunzo ya siku saba kwa mafundi mitambo wa radio za jamii 25 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.
Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo katika utendaji kazi wao.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Shirika hilo jijini Dar es salaam, mafunzo hayo yanagusa masuala yanayozunguka jamii namna ya kuyafanya kifanisi na kitaalamu ili kuweza kurusha matangazo yaliyomazuri kwa jamii ambayo yameanza Aprili 19 hadi Aprili 25 mwaka huu.
"Washiriki hawa wanatoka katika radio 25 za jamii zinazosaidiwa na shirika letu.Kubwa ni kuwapa mafundi mitambo hao elimu kuhusu namna ya kuifanya radio ya jamii kuwa bora wakati wa urushwaji wa matangazo kwa jamii husika,"imesema.
Imeongeza Unesco kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uswis (SDC) husaidia radio za jamii na mtandao wa radio za jamii (TADIO).
Ufadhili huo umelenga kuhakikisha wananchi wa Tanzania hasa wale wa vijijini wanafanya uamuzi sahihi kuhusu maisha yao kwa kupata taarifa sahihi kutoka redioni.
Afisa
Miradi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO), Rose Ngunangwa akifafanua jambo wakati wa mafunzo ya
kuwajengea uwezo mafundi mitambo wa radio za jamii 25 yaliyoandaliwa
na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)
yaliyoanza Aprili 19 hadi Aprili 25 mwaka huu.
Meneja
wa Huduma za Ufundi kutoka TBC, Mhandisi Yusuph Afidhu akizungumza na
washiriki kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo mafundi mitambo wa radio za
jamii zilizopo Tanzania Bara na Zanzibar.
Mkuu
wa Studio Redio ya TBC, Mhandisi Omary Salum akitoa mada kuhusu namna
ya studio inavyobidi kuwa ili kuweza kurusha matangazo kistadi wakati wa
mafunzo ya kuwajengea uwezo mafundi mitambo wa radio za jamii 25
yaliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO).
Baadhi
ya mafundi mitambo wa radio za jamii wakichangia mada kwenye mafunzo ya
kuwajengea uwezo kwa mafundi mitambo wa radio za jamii 25
yaliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO) yaliyoanza Aprili 19 hadi Aprili 25 mwaka huu.
Baadhi
ya mafundi mitambo wa radio za jamii wakiwa kwenye mafunzo ya vitendo
kwenye kituo cha TBC cha Tazara wakati mafunzo ya kuwajengea uwezo kwa
mafundi mitambo wa radio za jamii 25.
KUSOMA ZAIDI BODYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BODYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...