Na Mwandishi Wetu
Wasanii wa filamu nchi washauri kuheshimu na kutahmini mawazo na busara za wazee pindi wanapopata wasaa wa kukutana nao.

Rai hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Bi. Joyce Fissoo alipokaribishwa kutoa neno wakati wa tukio fupi la Msanii wa Bongo Movie Yvone Cherryl ‘‘Monalisa” kutoa shukrani kwa wajumbe wa Kamati ya Tamasha la Muziki na Sanaa za Maonesho Tanzania.

Fissoo alisema kuwa imekuwa ni desturi kwa baadhi ya vijana kuchukulia ushauri au mawazo yanayotolewa na wazee au watu wa makamu kuwa umepitwa na wakati hivyo hautakuwa na manufaa kwao.

“Nikuombe mwanangu Monalisa nenda ukawe balozi mwema, waanbie wenzako waenzi na kuheshimu busara za wazee, naamini kwa kufanya hivyo mtayaona mafanikio ya kazi zenu,”

Aidha mama Fissoo ameongeza kuwa Monalisa amekuwa msanii wa mfano wa kuigwa hasa katika nyanja ya maadili kitu ambacho wasanii wengi wanapaswa kuzingatia .
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bi. Joyce Fissoo akizungumza alipokuwa ameambatana na Msanii wa Filamu nchini Yvonne Cherrie maarufu kama Monalisa kwa ajili ya kutoa shukrani kwa wajumbe wa kamati ya tamasha la muziki na sanaa za maonesho jana jijini Dar es Salaam. Shukrani hizo zimetokana na wajumbe hao kumpa maneno ya kheri na busara msanii huyo hatimaye kurejea nchini na ushindi wa nafasi Msanii Bora wa Kike Afrika. 
Msanii wa Bongo Movie Yvone Cherry maarufu kwa jina la Monalisa akitoa neno la shukrani kwa wajumbe wa kamati ya tamasha la muziki na sanaa za maonesho jana jijini Dar es Salaam. Shukrani hizo zimetokana na wajumbe hao kumpa maneno ya kheri na busara msanii huyo hatimaye kurejea na ushindi wa nafasi Msanii Bora wa Kike Afrika.  Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Tamasha la Muziki na Sanaa za Maonesho Tanzania, Faza Lusozi Paul na kulia ni mama mzazi wa Monalisa, Bibi. Suzan Lewis.
Mwenyekiti wa Kamati ya Tamasha la Muziki na Sanaa za Maonesho Tanzania, Faza Lusozi Paul akizungumza jambo mara baada ya Msanii wa Bongo Movie Yvone Cherry maarufu kwa jina la Monalisa (wapili kulia) kutoa neno la shukrani kwa wajumbe wa Kamati ya Tamasha la Muziki na Sanaa za Maonesho Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Shukrani hizo zimetokana na wajumbe hao kumpa maneno ya kheri na busara msanii huyo hatimaye kurejea na ushindi wa nafasi Msanii Bora wa Kike Afrika. Wakwanza kulia ni mama mzai wa Monalisa, Bibi. Suzan Lewis.
Mwanamuziki mkongwe wa nyimbo za dansi nchini, Mzee King Kikii akitoa nasaha kwa Msanii wa Bongo Movie Yvone Cherry maarufu kwa jina la Monalisa (hayupo pichani) mara baada ya msanii huyo kutoa neno la shukrani kwa wajumbe wa Kamati ya Tamasha la Muziki na Sanaa za Maonesho Tanzania jana jijini Dar es Salaam. Shukrani hizo zimetokana na wajumbe hao kumpa maneno ya kheri na busara msanii huyo hatimaye kurejea na ushindi wa nafasi Msanii Bora wa Kike Afrika. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bi. Joyce Fissoo.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Bibi. Joyce Fissoo (waliokaa kushoto) na Msanii wa Bongo Movie Yvone Cherry maarufu kwa jina la Monalisa(wanne kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Tamasha la Muziki na Sanaa za Maonesho Tanzania jana Jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...