Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza Jamuhuri ya Cuba kwa kumaliza Uchaguzi wa Bunge salama wa kuwachagua Wajumbe wa Baraza Kuu la Nguvu ya Umma lenye Mamlaka ya kumchagua Rais wa Baraza la Taifa la Nchi hiyo.

Alisema uchaguzi huo uliofanyika Mnamo Tarehe 11 Machi, 2018,  ambapo Wajumbe wa Baraza la Taifa la Cuba walimchaguwa Bwana Miguel Diaz –Canel kuwa Rais wa Nchi hiyo aliyekuwa msaidizi wa Kiongozi wa Taifa hilo Bwana Raul Castro ulikuwa na amani na kushuhudiwa na Jumuiya za Kimataifa.

Balozi Seif Ali Iddi alitoa pongezi hizo wakati akizungumza na Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo Hernandes kwenye Makazi yake Jijini  Dar es salaam.

Alisema kufuatia kumalizika kwa uchaguzi  huo Tanzania na Cuba zitaendelea kupata wasaa zaidi wa kushirikiana katika masuala na sekta zilizoanzishwa ambazo ana matumaini ya kuendelezwa chini ya Rais huyo Mpya wa Cuba Bwana Maguel Diaz – Canel mwenye fikra za watangulizi wake waliolenga kuona ustawi wa Bara la Afrika unaimarika na kukua siku hadi siku.

Akitoa shukrani zake Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo Hernandes alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Cuba itaendelea kuiunga Mkono Tanzania hasa katika masuala ya Elimu na Afya.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Kulia akisalimiana na Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo alipofika kwenye Makaazi yake Jijini Dar es salaam kumpongeza kwa Cuba kumaliza Uchaguzi wa Rais salama.
Balozi Seif akitia saini Kitabu cha Wageni mara baada ya kukaribishwa kwenye Ubalozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Jijini  Dar es salaam.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanziabr Balozi Seif  Kulia na Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Prifesa Lucas Domingo  Kushoto wakibadilishana mawazo kwenye Makaazi ya Balozi wa Cuba Jijini Dar es salaam.
Balozi Seif na Profesa Lucan akiangalia baadhi ya Picha na matukio mbali mbali yaliyojiri kwenye Maktaba ya Ubalozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania.
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi Kulia na Mke wa Balozi wa Cuba Nchini Tanzania Mama Melyin Suazez Alvarez  Kati kati Wakimfanyia mzaha Mtoto wa Mke wa Balozi Huyo aitwae Evelyn Hernandes Suarez.
Balozi Seif akiagana na Mke wa Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Mama  Melyin Suarez Alvarez. Kati kati yao ni Balozi Lucas Domingo Hernandes na Mtoto wake  Evelyn Hernandes Suarez. Picha na – OMPR – ZNZ.

 KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...