Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameipongeza Jamuhuri ya Cuba kwa kumaliza Uchaguzi wa Bunge salama wa kuwachagua Wajumbe wa Baraza Kuu la Nguvu ya Umma lenye Mamlaka ya kumchagua Rais wa Baraza la Taifa la Nchi hiyo.
Alisema uchaguzi huo uliofanyika Mnamo Tarehe 11 Machi, 2018, ambapo Wajumbe wa Baraza la Taifa la Cuba walimchaguwa Bwana Miguel Diaz –Canel kuwa Rais wa Nchi hiyo aliyekuwa msaidizi wa Kiongozi wa Taifa hilo Bwana Raul Castro ulikuwa na amani na kushuhudiwa na Jumuiya za Kimataifa.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa pongezi hizo wakati akizungumza na Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo Hernandes kwenye Makazi yake Jijini Dar es salaam.
Alisema kufuatia kumalizika kwa uchaguzi huo Tanzania na Cuba zitaendelea kupata wasaa zaidi wa kushirikiana katika masuala na sekta zilizoanzishwa ambazo ana matumaini ya kuendelezwa chini ya Rais huyo Mpya wa Cuba Bwana Maguel Diaz – Canel mwenye fikra za watangulizi wake waliolenga kuona ustawi wa Bara la Afrika unaimarika na kukua siku hadi siku.
Akitoa shukrani zake Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo Hernandes alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Cuba itaendelea kuiunga Mkono Tanzania hasa katika masuala ya Elimu na Afya.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Kulia akisalimiana na
Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Profesa Lucas Domingo
alipofika kwenye Makaazi yake Jijini Dar es salaam kumpongeza kwa Cuba
kumaliza Uchaguzi wa Rais salama.
Balozi
Seif akitia saini Kitabu cha Wageni mara baada ya kukaribishwa kwenye
Ubalozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania Jijini Dar es salaam.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanziabr Balozi Seif Kulia na Balozi wa Jamuhuri ya
Cuba Nchini Tanzania Prifesa Lucas Domingo Kushoto wakibadilishana
mawazo kwenye Makaazi ya Balozi wa Cuba Jijini Dar es salaam.
Balozi
Seif na Profesa Lucan akiangalia baadhi ya Picha na matukio mbali mbali
yaliyojiri kwenye Maktaba ya Ubalozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini
Tanzania.
Mke
wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi Kulia na
Mke wa Balozi wa Cuba Nchini Tanzania Mama Melyin Suazez Alvarez Kati
kati Wakimfanyia mzaha Mtoto wa Mke wa Balozi Huyo aitwae Evelyn
Hernandes Suarez.
Balozi
Seif akiagana na Mke wa Balozi wa Jamuhuri ya Cuba Nchini Tanzania
Mama Melyin Suarez Alvarez. Kati kati yao ni Balozi Lucas Domingo
Hernandes na Mtoto wake Evelyn Hernandes Suarez. Picha na – OMPR – ZNZ.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...