Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema wakati umefika kwa kila Mwananchi mwenye sifa za uchangiaji damu kuanzia umri wa Miaka 18 hadi 65 uzito wa Kilogram 50 ajitokeze kujitolea kuchangia damu ili kuiepusha Jamii kukumbwa na upungufu wa damu salama Nchini ambao wakati mwengine huleta athari.

Alisema upungufu mkubwa wa Damu uliojitokeza Mwaka uliopita hasa katika Kipindi Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa mujibu wa Taarifa za uchangiaji Damu Salama katika Maabara za Mahospitali Zanzibar ulipelekea kwenda kuomba Damu Tanzania Bara.

Akizungumza katika Bonaza la Uchangiaji Damu Salama lililoandaliwa na Mkoa wa Kusini Unguja na kufanyika Dunga Wilaya ya Kati Balozi Seif Ali Iddi alisema kwa mujibu wa Takwimu zilizopo inaonyesha kwamba mahitaji halisi ni chupa 1,250 kwa Mwezi kwa matumizi ya kawaida Unguja na Pemba.

Balozi Seif alisema shughuli za uchangiaji wa damu salama  humgusa kila mwana jamii  hivyo ipo faida kubwa inayopatikana licha ya kuokoa maisha ya walio wengi ambao hupatwa na matatizo ya kiafya lakini pia humrahisishia Mtu kuweza kupima maradhi mbali mbali bure bila ya gharama sambamba na kuelewa afya yake.

Aliwaasa Wananchi kutambua umuhimu wa kuokoa maisha yao wenyewe wakiwa kama wana Jamii hasa wanapoelekea katika mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani  ambao wengi hushindwa kuchangia Damu kwa wakati  pale wanapokuwa na mgonjwa anayehitaji huduma hiyo kwa haraka.
 Wataalamu wa Kitengo cha Huduma  za Damu Salama wakianza zoezi la kuwapima Wananchi waliojitokeza kuchangia Damu kwenye Bonaza la Uchangiaji Damu la Mkoa Kusini Unguja lililofanyika Wilaya ya Kati Dunga.
Wananchi mbali mbali wakipata ushauri nasaha kutoka kwa Wataalamu wa Kitengo cha Huduma  za Damu Salama kabla ya kuchangia Damu kwenye Bonaza la Uchangiaji Damu la Mkoa Kusini Unguja.
Afisa uhamasishaji wa kuchangia Damu kutoka Jumuiya ya Wachangiaji Damu Zanzibar Bwana Bakari Mabarawa aliyenyanyua  mikono akimpatia maelezo Balozi Seif jinsi ya Kampeni ya Uchangiaji Damu Salama unavyofanywa katika maeneo mbali mbali Nchini.
Mmoja wa Mchangiaji Damu aliyejitokeza kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Bwana Sabri Yussuf Ali akichangia Damu kwenye Bonaza la Uchangiaji Damu la Mkoa Kusini Unguja lililofanyika Wilaya ya Kati Dunga.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na wananchi wakati wa kichangia Damu kwenye Bonaza la Uchangiaji Damu la Mkoa Kusini Unguja lililofanyika Wilaya ya Kati Dunga.
Picha na – OMPR – ZNZ.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...