Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
BALOZI wa India nchini Tanzania Sandeep Arya amewahimiza Watanzania kuchangia fursa za elimu ya juu inayotolewa katika nchi yao huku akifafanua mkakati walio nao ni kutoa elimu kwa wanafunzi 200,000 kutoka nje ya nchi na kuwasaidia kupata elimu bora na ufanisi kutoka vyuo mbalimbali nchini humo.

Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza fursa za kielimu zinazopatikana nchini India ambapo hafla hiyo ilihudhuriwa pia na viongozi wa Serikali, shule, vyuo na taasisi ya elimu ya juu.

Hivyo, amesema anawaalika watanzania kwenda kusoma nchini India ili kupata uzoefu na kukutana na wanafunzi kutoka nchi nyingine katika elimu ya juu katika vyuo vya nchini humo na kuongeza Tanzania na India wana urafiki wa muda mrefu na hiyo imesaidia Watanzania wengi kusoma nchini India .

"Kuna watanzania wengi ambao wamesoma kwenye vyuo vilivyopo nchini India na mchango wao katika maendeleo ya nchi ni mkubwa.Hivyo tunaendelea kuwakarabisha kwa wanaotoaka kusoma masomo ya elimu ya juu kusoma India , tunajivunia elimu bora ambayo inatolewa na yenye tija ya kuleta maendeleo,"amesema Balozi Arya.

Aidha amesema wanaotaka kwenda kusoma India wanaweza kupata taarifa kupitia tovuti ya www.studyinindia.gov.in portal.

Amefafanua kuwa elimu wanayoitoa ipo katika uhalisia katika masuala ya elimu, uchumi na jamii kwa ujumla na hivyo watanzania kusoma nchini India ni fursa ya kubadilisha sekta mbalimbali kutokana na elimu watakayoipata.

Kwa upande wake Mhitimu wa Symbiosis International (Deemed University)India Angelelda William amewahimiza vijana wa kitanzania kwenda kusoma kwenye chuo ambacho yeye amesoma kutokana na ubora wa elimu inayotolewa chuoni hapo. Amesema kwa atakayekwenda kusoma chuoni hapo hatajua ada ambayo anaitoa huku akisisitiza baada ya kuhitimu katika chuo hicho uwezo wake katika kufanya mambo ni mkubwa.

Kuhusu elimu inayotolewa nchini India amesema vyuo vingi vya nchini hiyo vimejikita kutoa elimu ya vitendo zaidi badala ya kuandika na sababu kubwa ni wanamuandaa mwanafunzi kufanya kazi kwa vitendo zaidi badala ya kuandika kwenye makaratasi.

”Nimesoma katika Chuo cha Symbiosis ambacho kimejikita kutoa elimu yenye ubora wa hali ya juu.Nitumie nafasi hii kuwaomba vijana wenzangu wanapofikia kwenda kusoma India basi chaguo lao la kwanza liwe kwenye chuo hiki maana nimekaa na nakijua vizuri,"amesema William.
 Balozi wa India nchini Tanzania Sandeep Arya akizungumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu ubora wa elimu ya juu unaotolewa na vyuo vya nchini India.
 Baadhi ya wadau mbalimbali wa elimu wakimsikiliza Balozi wa India nchini Tanzania Sandeep Arya wakati anazungumzia elimu ya juu inayotolewa nchini India
 Mhitimu wa Symbiosis International (Deemed)Univesity Angelelda Willim(kushoto) akiwa na Ofisa wa Ofa za Kimataifa na Mahusiano ya Wanafunzi wa Symbiosis(kulia)wakitoa maelezo kuhusu ubora wa chuo chao leo jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa Kituo cha Chanel Ten jijini Dar es Salaam Fred Mwanjala na Beatrice Erick wakipata maelezo kuhusu namna ya kujiunga na moja ya chuo cha nchini India.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...