Na Pamela
Mollel,Arusha
Benki ya
CRDB inatarajia kufanya mkutano wake wa ishirini na tatu(23)wa wanahisa wa
benki hiyo katika ukumbi wa Kimataifa wa AICC ulipo jijini Arusha na
kuhudhuriwa na watu zaidi ya Elfu moja.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei
alisema kuwa mkutano huo wa wanahisa unatarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi
huu
Dkt.Kimei
alisema kuwa Mkutano huo wa wanahisa wa benki ya CRDB utatanguliwa na semina
maalumu kwa wanahisa wa benki hiyo utakaofanyika tarehe 18 mwenzi huu ambapo
pamoja na mambo mengine wanahisa watapata fursa ya kufahamu mambo mbalimbali kibenki
Alisema kuwa
agenda za mkutano huo ni kupokea na kupitisha taarifa za fedha na ripoti za
wakurugenzi kwa mwaka uliopita tarehe 31 mwezi Disemba 2017,kuhidhinisha
taarifa maalumu ya gawiyo wa mwaka ,kuchagua wajumbe wa bodi ,kuhidhinisha
uchaguzi wa wakaguzi wa hesabu wanaokupalika kisheria
Dkt Kimei
alitoa rai kwa wanahisa wa benki hiyo kuuhudhuria kwa wingi katika mkutano huo
mkuu huku akiongeza kuwa kwa mwanahisa ambaye hataweza kuudhuria anahaki ya
kuchagua mwakilishi au wawakilishi kuudhuria na kupiga kura kwa niaba yake.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei akizungumza na vyombo vya
habari jijini Arusha leo ,kuhusu mkutano mkuu wa ishirini na tatu wa
Wanahisa unaotarajia kuanza rasmi tatehe 18 na 19 utakaohudhuriwa na
wanahisa zaidi ya Elfu moja katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa
AICC uliopo jijini Arusha(Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei kushoto,kulia ni Mkurugenzi wa mikopo James Mabula kulia
Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa masoko wa CRDB Jadi Ngwale,kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei
Waandishi wa habari wakiwa wanafanya mahojiano ya kina kuhusu mkutano huo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...