Na Pamela Mollel,Arusha

Benki ya CRDB inatarajia kufanya mkutano wake wa ishirini na tatu(23)wa wanahisa wa benki hiyo katika ukumbi wa Kimataifa wa AICC ulipo jijini Arusha na kuhudhuriwa na watu zaidi ya Elfu moja.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei alisema kuwa mkutano huo wa wanahisa unatarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi huu

Dkt.Kimei alisema kuwa Mkutano huo wa wanahisa wa benki ya CRDB utatanguliwa na semina maalumu kwa wanahisa wa benki hiyo utakaofanyika tarehe 18 mwenzi huu ambapo pamoja na mambo mengine wanahisa watapata fursa ya kufahamu mambo mbalimbali kibenki

Alisema kuwa agenda za mkutano huo ni kupokea na kupitisha taarifa za fedha na ripoti za wakurugenzi kwa mwaka uliopita tarehe 31 mwezi Disemba 2017,kuhidhinisha taarifa maalumu ya gawiyo wa mwaka ,kuchagua wajumbe wa bodi ,kuhidhinisha uchaguzi wa wakaguzi wa hesabu wanaokupalika kisheria

Dkt Kimei alitoa rai kwa wanahisa wa benki hiyo kuuhudhuria kwa wingi katika mkutano huo mkuu huku akiongeza kuwa kwa mwanahisa ambaye hataweza kuudhuria anahaki ya kuchagua mwakilishi au wawakilishi kuudhuria na kupiga kura kwa niaba yake.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha leo ,kuhusu mkutano mkuu wa ishirini na tatu wa Wanahisa unaotarajia kuanza rasmi tatehe 18 na 19 utakaohudhuriwa na wanahisa zaidi ya Elfu moja  katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC uliopo jijini Arusha(Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei kushoto,kulia ni Mkurugenzi wa mikopo James Mabula  kulia 
Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa masoko wa CRDB Jadi Ngwale,kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei
Waandishi wa habari wakiwa wanafanya mahojiano ya kina kuhusu mkutano huo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...