Mwenyekiti wa bodi ya benki ya biashara ya Mkombozi Method Kashonda akizungumzia jinsi benki hiyo ilivyofanikiwa kupata faidi baada ya kodi ya shilingi bilioni 1.44 kwa mwaka 2017 kutoka shilingi bilioni 1.05 ilivyokuwa mwaka 2016. Sawa na ongezeko la asilimia 37.1  katika mkutano mkuu wa mwaka wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Bank ya Mkombozi, George Shumbusho akizungumzia matarajio ya benki kuanza kutumia mfumo wa kimataifa wa ripoti za fedha wa IFRS (International Financial Report Standard), ili kumuhakikishia mteja anapata huduma za mkopo kwa uhakika.
Mhashamu baba askofu mkuu wa jimbo Katoliki la Dodoma, Beatus Kinyaiya akifafanua juu ya mkakati wa benki ya mkombozi wa kushawishi waumini wa kanisa katoliki kununua hisa kwa wingi ambapo gawio la mwaka 2017 limeongeza kwa shilingi 5 sawa na shilingi 25 kwa hisa kutoka gawio la shilingi 20 ilivyokua mwaka 2016.
Makamu mwenyekiti wa bodi ya Mkombozi Profesa Marcellina M. Chijoriga akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo.
Wanahisa wa benki ya Mkombozi wakifuatilia mkutano kwa makini. 
Picha ya pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...