*Apiga marufuku mwanafunzi kuchapwa viboko shuleni, atoa mbinu za ufundishaji
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
KATIBU wa Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania Winfrida Rutahinfwa ametoa maagizo kwa Walimu wakuu na Wakuu wa shule nchini kutoogopa kuwachukulia walimu ambao watabainika wanakiuka nidhamu ya utumishi hata kama walimu hao watakuwa ni wake wa viongozi wa ngazi za juu Serikali.
Pia amewaagiza walimu kubuni mbinu za kufundisha wanafunzi ili wafaulu kwenye masomo huku kwa walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam hasa wa Shule za Sekondari kujikita katika kufundisha wanafunzi ili wafaulu kwani kwa sasa shule za mkoa huo zinafanya vibaya kwenye matokeo ya mtihani.
Rutahinfwa amesema hayo leo wakati anazungumza na walimu wakuu wa shule za msingi, Wakuu wa shule za sekondari, maofisa elimu na viongozi wa ngazi mbalimbali wa sekta ya elimu mkoa wa Dar es Salaam na hasa wa Manispaa ya Ilala jijini.
"Mwalimu mkuu wa shule ya msingi na mkuu wa shule sekondari ndiko mamkalaka ya nidhamu yanakoanzia kwa maana kwenye ngazi za shule,hivyo nitoe mwito walimu wakuu na wakuu wa shule chukueni hatua kwa walimu wanapokosea.
"Mwalimu hata akiwa mke wa kiongozi achukuliwe hatua pale anapokiuka nidhamu,anapokuwa kwenye majukumu yake ni mwalimu na akirudi nyumbani ndio atabaki kuwa mke wa kiongozi.
"Hivyo hakuna sababu ya kuogopa kuchukua haua kwasababu mwalimu aliyekosea ni mke wa mkubwa.Tufuate sheria na kanuni za utumishi wa umma na zile za Tume ya Utumishi wa Walimu Tanzania.Anayekosea aanywe, apewe karipio na akiendelea achukuliwe hatua zaidi,"amesema Rutahinfwa .
Baadhi
ya walimu walimi wakuu wa shule za msingi,wakuu wa shule za
sekondari,waratibu wa elimu na maofisa elimu mkoa wa Dar es Salaam
wakiwa wamesimama kumkaribisha Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu
Tanzania Winfrida Rutahinfwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...