Mkurugenzi wa Kampuni ya Kilifair Ltd ,Tom Kunkler akizungumza mbele ya waandishi kuhusu tukio la Maonesho ya Kimatifa ya Utalii ya KAribu Kilifair yanayotaraji kufanyika mjini Moshi ,June 1 hadi 3 mwaka huu. 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini .

MAKAMPUNI 380 yanayojishughulisha na Utalii yanataraji kushiriki Maonesho ya Kimataifa ya Karibu Kilifair huku kampuni ya Kilifair Ltd inayoratibu maonesho hayo ikitangaza kuandaa safari za kifamilia zitakazoshirikisha watu kutoka nchi mbalimbali Duniani kujionea vuvitio vya utalii kwa lengo la kuvitangaza kimataifa.

Maonesho ya kimataifa ya Utalii yaliyopewa jina la Karibu Kilifair yanafanyika kwa mwaka wan ne sasa yakiwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya Utalii wa Tanzania na nje ya nchi ,kwa lengo la kutangaza bidhaa mbalimbali za Utalii ikiwemo vivutio mbalimbali.

Kwa mara ya kwanza Kampuni ya Kilimanjaro SIR inayojishughulisha na ukoaji wa wageni waliopata matatizo katika maeneo yenye miinuko kama Mlima Kilimanjaro na Meru inataraji kushiriki katika maonesho hayo huku Shirika la ndege la Ethiopian Airlines likitangaza kutumia maonesho hayo kutangaza vivutio vya Utalii kwa wageni watakaosafiri na ndege wa shirika hilo.

Maonesho ya Karibu Kilifair yanayoratibiwa na Kampuni ya Kilifair Ltd awali yalijukiana kama Kilifair yakidhaminiwa na Kampuni mbalimbali za ndani na nje ya nchi .
 Viongozi wa Kampuni ya uokoaji ya Kilimanjaro SIR wakifuatilia maelezo juu ya manesho hayo yaliyokuwa yakitolewa kwa wanahabari. 
 Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Kilifair inayoratibu maonesho ya Karibu Kilifair ,Dominic Shoo akizungumzia tukio hilo kubwa la Kitalii. 
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Uokoaji ya Kilimanjaro SIR ,Ivan Brown akizungumza wakati wa kikao na wanahabri kuhusu tukio hilo. 
 Meneja Mauzo wa Shirika la Ndege la Ethiopian Airlines ,Fitsimt Dejene ambao ni miongoni mwa wadhamini wa Maonesho ya Kimataifa ya Karibu Kilifair yanayotaraji kufanyika mjini Moshi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...