Masheikh 11 wa madhahebu ya Shia Ithna Sheria katika mikoa ya Mwanza, Simiyu, Kagera,Tabora, Kigoma, Dodoma na Katavi wamepewa vitendea kazi vyenye thamani ya shilingi milioni 80. 

Vitendea kazi hivyo pikipiki aina ya Freedom vilikabidhiwa jana kwa mashaeikh hao na mlezi wa taasisi ya The Bhakhiyatullah Foundation ya jijini Mwanza Alhaji Sibtain Meghjee hafla iliyofanyika kwenye ofisi za Bilal Muslim Mission of Tanzania Mwanza.

Akikabidhi pikipiki hizo Sibtain ambaye ni Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foundation aliwataka wakazitumie kutembelea jamii na kuibua kero na changamoto zinazoikabili bila kujali imani zao za dini kwenye maeneo yao na kisha kutoa taarifa na maoni ya utatuzi wa changamoto hizo.

“Pikipiki hizi mmekabidhiwa na nyaraka zote mkazitumie vizuri kwa kuhudumia jamii na isiwe kwa waislamu tu bali na waumini wa dini zote na sisi tunatoa huduma bila kubagua.Mzitumie vizuri ili na wengine waweze kupata lakini mkishindwa mtasababisha wakose,”alisema Meghjee na akawataka watoe mrejesho wa matokeo chanya yatakayopatikana kwenye jamii baada ya miezi sita tangu wakabidhiwe pikipiki hizo.

Wakizungumza baada ya kupokea msaada huo baadhi ya masheikh walisema mbali na kuzitumia kuibua changamoto kwa waumini wao na jamii ya waumini wa dini zingine zitawasaidia kuwaingizia kipato.

“ Tofauti na zamani sasa kazi itakuwa rahisi kutokana na vipandwa (vifaa) hivi vya usafiri ambavyo vitaturahishia kuwafikishia ujumbe wa Allah (Mungu) waumini wetu lakini pia tutawafikia kwa urahisi watu mbalimbali kwenye maeneo yetu na kuibua kero na changamoto zao. Tunawashukuru wafadhili waliotovitoa,”alisema Sheikh Hussein Thuqumali wa TBF.
Mwenyekiti wa taasisi ya The Bakhiyatullah Foundation (TBF) ya jijini Mwanza Sheikh Hashim Ramadhan akizungumza na baadhi ya masheikh kabla ya kuwakabidhi pikipiki kwa ajili ya usafiri. Kulia ni mfadhili aliyetoa pikipiki hizo Sibtain Meghjee wa The Desk & Chair Foundation tawi la Tanzania na mwenye kilemba ni Maulana (waliokaa) wa pili kushoto Sayyed Amir Abass Bakri.
Sheikh Hussein Thuqumali wa TBF akitia saini (mkataba) wa kumilikishwa pikipiki wanaoshuhudia ni Maulana Sayyed Amir Abbas Bakri katikati na Mwenyekiti wa The Bakhiyatullah Foundation (TBF) Sheikh Hasim Ramadhani.
Sheikh Daud Daud wa Lamadi Simiyu akipokea hati za pikipiki aliyokabidhiwa kutoka kwa Mwenyekiti wa The Desk & Chair Foundation Alhaji Sibtain Meghjee kulia.
Masheikh wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa pikipiki za usafiri kutoka taasisi ya The Bakhiyatullah (TBF) pikipiki hizo zimetolewa na The Desk & Chair kwa masheikh hao ili kuwasaidia usafiri waweze kuibua kero na changamoto kwenye jamii. picha Baltazar Mashaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...