JOSEPH MPANGALA,MTWARA
Serikali imesema imekamilisha ujenzi wa Bomba la gas utakoyoiwezesha kampuni ya kuzalisha saruji ya Dangote iliyopo mkoani Mtwara ambayo inataraji kuzalisha umeme wa megawatts 35 ambazo zitatumika kwa ajili ya matumizi ya Kiwanda Hicho.
Akiongea mara baada ya kutembelea plants ya Kuzalisha umeme ambayo inatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi huu waziri wa Nishati Dk.Medard Kalemani amesema kuwa tayari serikali ipo tayari kwa ajili ya kutoa nishati ya Gas ili kampuni ya Dangote  kuweza kuzalisha umeme.
“Na mm nawaambia tena TPDC wakichelewa baada ya mezi kuisha wakumbushe kwa barua ili lieleweke kama nani anayechelewa lakini sio wanachelewa kwa makusudi bali wanamaandalizi yao wenyewe lakini sisi kwa upande wetu kama serikali tupo tayari hata kama wangetaka leo jioni watachukua gas ili waendelee kwa hiyo nilitaka kuliweka hili Vizuri kwamba tumeendelea vizuri kati ya TPDC na Dangote”
Lakini naye Mhandisi wa kampuni ya BQ Cntractors Limited John Bura anasema Dangote ataendelea kununua nishati ya Gas zaidi ambapo kufikia mwisho wa mwezi June Mtambo itakuwa umekamilika tayari kwa kuanza kwa uzalishaji wa Saruji ambapo ni umbali wa kilomita 2.7 kufikia kiwandani
Aidha ameongeza kuwa kwa sasa uzalishaji wa saruji ni asilimia 50 lakini kukamika kwa ujenzi huo kutawezesha kampuni ya dangote kuzalisha saruji mifuko lakimoja na Nusu kwa siku.

Meneja Mkuu wa GASCO Mhandisi Baltazari T.Mrosso akimuonesha waziri wa Nishati Dk.Medard Kelamani Bomba la Gas linalopeleka Nishati hiyo katika Kiwanda cha Umeme cha Dangote.


Waziri wa Nishati Dr.Medard Kelamani akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kiwanda cha kuchakata Gas na Bomba la Gas Linaloelekea Kiwanda cha saruji Cha dangote.
Waziri wa Nishati na madini Dr Medard Kelamani akiongea na Mkurugenzi wa kiwanda cha Dangote Alhaji Sada ladeubaki mara baada ya kutembelea ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha umeme utakaopelekwa katika kiwanda cha Dangote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...