Na Hassan Mabuye, Wizara ya Ardhi
Serikali
yamaliza mgogoro wa mpaka kati ya mkoa wa Manyara na Tanga katika
wilaya za Kiteto na Kilindi uliodumu kwa zaidi ya miaka 20.
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe William
Lukuvi ambaye amesema moja ya sababu kubwa za kuwepo kwa mgogoro huo ni
baadhi ya wapimaji mipaka waliokuwepo wakati huo kuhongwa na kupindisha
mpaka.
Mgogoro
huu uliwasilishwa kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Kassim Majaliwa wakati alipofanya ziara yake mwezi januari mwaka
2017 ambapo wananchi walifikisha malalamiko ya mgogoro huo ambao
umegharimu maisha ya watu wengi na mauaji ya mara kwa mara.
Waziri
Mkuu alimtaka wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
kushirikiana na Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI kuunda timu ya
wataalamu ambao walianza kazi ya upimaji mwezi Machi 2017 ambao walipima
mpaka huo kwa usahihi japo na wao walitaka kuhongwa pesa kutoka kwa
baadhi ya watu hata hivyo walizikataa.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe William Lukuvi akiongea na
wananchi wa wilaya za Kiteto na Kilindi waliohudhuria katika mkutano
wakati akiwatangazia kuhusu Serikali kumaliza mgogoro wa mpaka wa wilaya
hizo mbili.
Eneo la mpaka wa Kiteto na Kilindi ambalo lilikuwa na mgogoro
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe William Lukuvi akisalimiana
na wakazi wa wilaya za Kiteto na Kilindi wenyenyuso za furaha mara
baada ya kumalizika kwa mgogoro huo.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Suleiman Jafo akisalimiana na
wakazi wa wilaya za Kiteto na Kilindi wenyenyuso za furaha mara baada ya
kumalizika kwa mgogoro huo.
Baadhi ya wananchi wa wilaya za Kiteto na Kilindi waliohudhuria katika
mkutano wa utatuzi wa mgogoro kati ya wilaya hizo wakifuatilia kwa
makini maamuzi ya utatuzi wa mgogoro huo.
wananchi
wa wilaya za Kiteto na Kilindi waliohudhuria katika mkutano wa utatuzi
wa mgogoro kati ya wilaya hizo wakifuatilia kwa makini maamuzi ya
utatuzi wa mgogoro huo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...