Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
UONGOZI wa United Bank for Africa(UBA) umesema umejipanga kuendelea kutoa huduma bora za kifedha kwa Watanzania huku ukifafanua kukua kwa teknolojia kumeifanya benki yao kutoa huduma zake kwa njia ya mtandao na kuwafikia wateja wengi zaidi.

Pia umeeleza mikakati yao katika kuhakikisha wanashiriki kuleta maendeleo nchini na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Tano.Pia umewahimiza wananchi umuhimu wa kuwa na Kitambulisho cha Taifa kwani vinarahisisha kwa wanaohitahi kufungua akaunti benki.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na uongozi wa UBA wakati wanazungumza na waandishi wa vyombo vya habari kuhusu mafanikio, malengo na mikakati yao katika utoaji wa huduma za kibenki nchini. Pia UBA umekutana na wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM).

Mtendaji Mkuu wa UBA nchini Tanzania Chris Byaruhanga ,amesema tangu kuanzishwa kwa benki hiyo miaka 75 iliyopita nchini Nigeria na kufungua matawi katika nchini mbalimbali ikiwemo Tanzania wamepata mafanikio makubwa na benki hiyo imekuwa chachu ya maendeleo katika Bara la Afrika.

Amefafanua kwa Tanzania UBA imeendelea kujiimarisha katika kutoa huduma bora za kibenki na imekuwa mstari wa mbele kuchangia shughuli za kimaendeleo na kubwa zaidi uwepo wa benki hiyo umesaidia kutoa ajira kwa Watanzania.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo Brendansia Kileo (kulia) akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati akizungumzia mipango mbalimbali ya UBA. Wengine ni Mkuu wa Mahusiano ya ndani na nje wa UBA Nasir Ramon(kushoto) na Mtendaji Mkuu wa UBA nchini Tanzania Chris Byaruhanga(katikati).
Mtendaji Mkuu wa UBA nchini Tanzania Chris Byaruhanga (katikati) akizungumzia mafanikio ya benki hiyo kwa waandishi wa habari nchini.Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo Brendansia Kileo na Mkuu wa Mahusiano ya ndani na nje wa UBA Nasir Ramon(kushoto)
Mkuu wa Mahusiano ya ndani na nje wa UBA Nasir Ramon (kushoto)akizungumzia mchango wa benki hiyo katika kuchangia maendeleo ya nchi za Afrika ikiwamo Tanzania.Kati kati ni Mtendaji Mkuu wa UBA nchini Tanzania Chris Byaruhanga na kulia ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo Brendansia Kileo
Mmoja ya maofisa wa UBA akielezea ubora wa kadi ya benki hiyo kwa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha(IFM) leo jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...