Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) imeendesha kikao kazi cha wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Shinyanga na Mwanza kwa ajili ya kuhamasisha kazi na majukumu ya TFDA na kujadiliana kwa pamoja mikakati ya Mamlaka ya kupambana na bidhaa duni na bandia katika soko na namna bora ya kushirikisha wananchi katika udhibiti na hatimaye kuhakikisha kuwa wanatumia bidhaa bora, salama na fanisi ili kumlinda mwananchi. 

Kikao kazi hicho kimefanyika Jumatatu Mei 21, 2018 katika ukumbi wa mikutano wa TFDA Kanda ya Ziwa uliopo Buzuruga jijini Mwanza ambapo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella. 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi hicho cha siku moja Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi.Agnes Sitta Kijo, alisema kikao hicho kinahusu uhamasishaji wa Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Sura 219.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu alisema kuwa, TFDA itaendelea kufuatilia, kuondoa na kuteketeza bidhaa ambazo hazikidhi vigezo vya ubora, usalama na ufanisi ili kuepusha bidhaa duni na bandia  kutumika ambapo amewahimiza Wahariri na Waandishi kufikisha elimu watakayoipata kwa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela akifungua kikao kazi kati ya TFDA, wahariri na waandishi wa vyombo vya habari wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa TFDA Kanda ya Ziwa, Mwanza tarehe 21 Mei, 2018.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo akitoa maelezo ya utangulizi wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kati ya TFDA, Wahariri na Waandishi wa vyombo vya habari wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga kilichofanyika katika ukumbi wa TFDA Kanda ya Ziwa, Mwanza tarehe 21 Mei, 2018. Kikao kazi hiki kilihusu uhamasishaji wa Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Sura Na.219.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari Maelezo, Bi. Zamaradi Kawawa akieleza wajibu wa waandishi na wahariri wa habari katika kuleta ufanisi wa utekelezaji wa Sheria ya Chakula Dawa na Vipodozi Sura Na. 219.
Mkurugenzi wa Dawa na Bidhaa Nyongeza wa TFDA, Bw. Adam Fimbo akifafanua jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba na vitendanishi nchini kwa wahariri na waandishi wa vyombo vya habari wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga (hawapo pichani).
Mkurugenzi wa Uendelezaji Huduma wa TFDA, Bw. Chrispin Severe, akieleza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu Dira Dhima na majukumu ya TFDA kwa wahariri na waandishi wa vyombo vya habari wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga. 
Mada kuhusu utambuzi wa dawa bandia na duni ikitolewa wakati wa kikao kazi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...