Na Rhoda Ezekiel Kigoma, 

WAKULIMA wilayani Kakonko mkoani Kigoma, wametakiwa kulima kilimo cha biashara na kuachana na kilimo cha kujikimu wenyewe ili kuweza kuondokana na umasikini.

Mwito huo ulitolewa jana katika Kijiji cha Kiga wilayani hapo na Ofisa Kilimo wa Mkoa wa Kigoma, Josephu Lubuye wakati wa ugawaji wa mashine ya kuchakata Muhogo kwa kikundi cha Mwendo wa saa, iliyo tolewa na Shirika la BTC kupitia mradi wa kilimo wa ENABEL unaotekelezwa na Serikali ya Ubelgiji na Tanzania.

Lengo ni kuendeleza kilimo cha muhogo na maharage kwa kuwakopesha wakulima mashine na kuwapatia mafunzo ya namna ya kulima kitaalamu.

Hivyo Lubuye amesema wakulima wanatakiwa kubadilika na kuanza kilimo cha biashara na mashine hiyo waliyoipata itumike kuchakata mazao mengi ya mihogo waliyolima kutokana na maombi na aandiko lao la kuomba mashine ya kuchakata mihogo.

Amesema hiyo itaongeza uzalishaji wa zao hilo kwa wingi ili wakulima wengine wajifunze kupitia kikundi hicho kutokana na uzalishaji watakaoufanya kupitia mafunzo ya kilimo cha biashara waliyo yapata kuongeza uzalishaji na ubora.

Akikabidhi mashine hiyo yenye thamani ya Sh.milioni mbili na yenye uwezo wa kuzalisha kilo 700 kwa saa moja na hufanya kazi kwa muda wa saa nane, Mkuu wa wilaya ya Kakonko kanali Hosea Ndagala amewataka wakulima kuacha kuuza mazao ambayo hayajaongezwa thamani.
 Mkuu wa wilaya ya Kakonko kanali Hosea Ndagala akikabidhi  mashine  ya kuchakata muhogo,yenye thamani ya Sh.milioni mbili na yenye uwezo wa kuzalisha kilo 700 kwa saa moja.DC Ndagala amekabidhi hiyo mashine ya kuchakata Muhogo kwa kikundi cha Mwendo wa saa, iliyo tolewa na Shirika la BTC kupitia mradi wa kilimo wa ENABEL unaotekelezwa na Serikali ya Ubelgiji na Tanzania.
 Sehemu ya shamba ka Muhogo. 
 Mkuu wa wilaya ya Kakonko kanali Hosea Ndagala akitumbukiza muhogo kwenye mashine ya kuchakata muhogo,ili kujionea ufanyaji wake kazi,mashine hiyo ina uwezo wa kuzalisha kilo 700 kwa saa moja.
Mihogo ilioandaliwa tayari kwa kuchakatwa na mashine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...