Kampuni ya Bima ya Afya ya AAR imewafuturisha wazee wanaotunzwa katika ‘Kituo cha TUSHIKAMANE PAMOJA cha jijini Dar es Salam na kuwapa msaada wa vitanda kama sehemu ya mchango wao katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Mkuu wa Itifaki wa BAKWATA, Shekh Mohammed Nassor akiambatana na viongozi wengine wa kidini waliongoza futari hiyo, iliyofanyika jana jioni, Juni 13, 2018 katika Ofisi za Makao Makuu ya AAR yaliyoko Mikocheni jijini Dar.

Akizungumza katika hafl hiyo, Shekh Mohamed ambaye ndio alikuwa mgeni rasmi, aliwapongeza AAR kwa kuwajali watu wenye uhitaji hususan wazee ambao alisema wanahitaji uangalizi maalum na faraja. 

Aidha, aliitaka jamii kwa ujumla kushiriki katika kutatua matatizo yanayowakabili wazee, akifafanua kuwa hata Mtume Muhammad (S.W.A) alionesha mfano katika hili akieleza kuwa, “Kama kijana atamheshimu mzee wakati wa umri wake, Mwenyezi Mungu atamteulia mtu atayemheshimu na kumjali wakati wa uzee wake pia.”

“Tunapotumia mwezi huu mtukufu wa Ramadhani kutafakari afya za roho zetu, tunapaswa kuhakikisha mazingira ya upendo na kuwajali wenye mahitaji maalum na hata wapita njia. Ninawapongeza AAR kwa kujali hali za wazee ambao ni kisima cha busara ambazo kama taifa tunaweza kuzitumia kuepuka migogoro isiyo ya lazima,” alisema Shekhe Mohammed.
 Mkuu wa Itifaki wa BAKWATA, Shekh Mohammed Nassor akizungumza na Wazee wa Kikundi cha Tushikame Pamoja kilichohudhuria Futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Bima ya AAR.
  Mwenyekiti wa Kikundi cha Tushikame, Bi. Rose Mwapachu akitoa shukrani kwa Uongozi wa Kampuni ya AAR kwa kuwakaribisha Futari hiyo pamoja nakusaidia baadhi ya vitu kama Vitanda.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya AAR, Bi. Violet Modichai akikabidhi baadhi ya vifaa kwa Wazee hao wa Kikundi cha Tushikame kilichopo Kwembe.
Sehemu ya Wazee wa Tushikame Group waliohudhuria Futari iliyoandaliwa na Kampuni ya AAR kwenye Makao Makuu yaliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...