Airtel yatangaza huduma mpya mbili, yatamba kuendelea kuboresha huduma zake kwendana na teknolojia

Kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania imehaidi kuendelea kutoa huduma bora na za kisasa kwa wateja wake. Hii ni kutatua kero na changamoto ambazo zimekuwa zikiikumba sekta ya mawasiliano hapa nchini.

Akiongea jijini Dar es Salaam jioni baada ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo kwa wateja na washirika wake, Mkurugenzi wa Biashara kwa wateja maalum Airtel Tanzania Boniface Bwambo alisema kampuni hiyo itaendelea kutoa huduma bora na za kisasa ili kukidhi matakwa ya wateja wake pamoja na kuongeza pato kutoka na huduma zake kwenye kipindi hiki ambacho ushindani umekuwa mkubwa kwenye sekta ya mawasiliano.

Bwambo alisema baadhi ya bidhaa mpya zinazotolewa na kampuni hiyo ili kwenda na wakati ni fixed portfolio ambayo huwapa wateja nafasi ya kufurahia huduma ya mtandao ya kasi ya Fiber Solutions, Line Solutions na Co-Location Solutions. Huduma hizi ni suluhisho kwa biashara za mtandaoni, inapatikana kwa gharama nafuu katika vifurushi zinazotolewa na Airtel.

Bwambo alisema hayo wakati wa futari iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam. ‘Mwezi mtukufu wa Ramadhani ni kipindi muhimu sana kwa waumini wa dini ya Kislam duniani kote. Kwa kutambua umuhimu huo, sisi Airtel tumeona ni Faraja kukutana hapa siku ya leo na kufuturu kwa pamoja. Hii ni moja ya njia nzuri pia kukutana na wateja na kuonyesha tunawajali. Vile vile, kwa kukutana pamoja hapa inatoa fursa ya kuzungumza na kuonyesha baadhi ya bidhaa zetu kwa wateja wetu, aliongeza  Bwambo.

‘Ni furaha sana kuwa nasi zote hapa. Ni furaha zaidi kuweza kutambua kuwa sisi Airtel tunatoa huduma zaidi ya mawasiliano. Kwa kuongea tu ni kwamba wengi wanajua huduma yetu ya Airtel Money ni kutuma na kupokea fedha na kununua au kulipia bidhaa. Lakini vile vile imeenda zaidi kwa kuweza kukusanya mauzo au mapato kwa wateja na kupeleka moja kwa moja kwenye akaunti yake ya benki. Kwa sasa mfanya biashara hana haja ya kutoka kukusanya mauzo ua mapato kwa sisi kupitia Airtel Money tufanya kazi hio na ndio sababu tunasema Airtel Money ni salama na njia nafuu ya kuweka na kutunza fedha. Alisema Bwambo .

Kwenye tukio la futari hiyo alikuwepo pia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Tanzania Sanjay Rughani. Alipongeza kampuni ya Airtel kwa kutambua umuhimu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani na pia kwa kutoa huduma bora na nafuu kwa wateja wake.

 ‘Airtel inafanya vizuri kwa kuboresha huduma zake kila siku ili kwenda na wakati kitu ambacho ni muhimu kwa wateja na washirika wake kama sisi. Kuja kwangu hapa leo kumeweza kunipa na kutambua huduma na bidhaa mpya kutoka Airtel ambazo nilikuwa sina taarifa nazo hapa awali. Hii ni jambo la kupongezwa sana, alisema Rughani.

On her side the Administration and Project Manager of the National Industrial and Commercial (NIC) Bank, MsBadriaLema, said out of enjoying sharing iftar with the Airtel staffs and other people, she gets a chance to know other services offered by the company especially Airtel Money profit distribution.

Kwa upande, Meneja Utawala na miradi wa benki ya NIC Tanzania Badrial Lema alisema ni furaha kubwa kuungana na wafanya kazi wa Airtel Tanzania kushiriki futari ya leo. ‘Nimefurahi sana kukutana na wafanyakazi wa Airtel na wageni wengine waalikwa. Ni tukio la iana yake kwani nimeweza kupata marafiki wapya na kuongeza ufahamu juu ya huduma zinazotolewa na Kampuni ya Airtel Tanzania.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Airtel Tanzania akimkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Tanzania Sanjay Rughani wakati wa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam. Kati kati ni Mkurugenzi wa Biashara Airtel Tanzania Rohit Tandon.
 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Airtel Tanzania akimkaribisha moja ya wageni waalikwa wakati wa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam. Kati kati ni Mkurugenzi wa Biashara Airtel Tanzania Rohit Tandon
 Mkurugenzi Mtendaji Airtel Tanzania Sunil Colaso akiongea na wafanya kazi wa kampuni hiyo, wateja na wageni waalikwa wakati wa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Tanzania Sanjay Rughani akiongea na moja ya wageni waalikwa wakati wa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam. Kati kati ni Mkurugenzi Mtendaji Airtel Tanzania Sunil Colaso.

 Mkurugenzi wa Biashara kwa wateja maalum Boniface Bwambo akiongea na wafanyakazi wa kampuni hiyo, wateja na wageni waalikwa wakati wa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Standard Tanzania Sanjay Rughani akiongea na Mkurugenzi wa Biashara Airtel Tanzania Rohit Tandon wakati wa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Airtel kwa wateja na washirika wake jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...