Na Anthony Ishengoma WAMJW.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa unaonesha kuwa kati ya asilimia 7 na 16 ya wanawake wote duniani ni Wajane.  

Jamii imetakiwa kuendeleza mipango na kuongeza juhudi zaidi katika kukabiliana na vitendo vya ukatili, unyanyasaji na kuwainua wajane ili wapate uwezo wa kiuchumi wa kuzihudumia familia na wategemezi wao kwa kuwa ndiyo muhimili pekee wa familia iliyoachwa.

Akiongea kwa niaba ya Mgeni rasmi wa kongamano la Wajane liliofanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa Bi. Honoratha Rwegasira amepongeza juhudi za wadau wa maendeleo na serikali katika kuwasaidia wajane kuleta usawa wa kinjisia na kuinua ushiriki wao katika ngazi za kutoa maamuzi.  

Aidha Bi.Rwegasira ameitaka jamii kuacha mila potofu kama vile kunyanganya mali mjane, kuozesha watoto wa kike katika umri mdogo, kurithi wajane na nyingine zote zinazoweza kumdhoofisha mwanamke katika jitihada zake za kujikwamua kifikra, kiutamaduni, kiuchumi,kijamii na kisiasa.
 Mkurugezi  Msaidizi  Idara ya Jinsia, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Mwajuma Magwiza akitoa hutuba yake kwenye  Kongomano la Wajane lililofanyika leo Mjini Dodoma.
 Afisa Mwandamizi  Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi .Sirivia Siliwa  akitoa mada kuhusu Chimbuko la  Siku ya  Wajane Duniani wakati wa Kongomano la Wajane lilifanyika leo Mjini Dodoma.
 Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma  Bi. Honoratha Rwegasira  akitoa hutuba ufunguzi  kwa niahaba ya Mgeni rasmi wakati wa  Kongomano la Wajane lililofanyika leo Mjini Dodoma.
Wajane wa Mkoa  wa Dodoma wakiwa kwenye  Kongomano la Wajane lililofanyika leo Mjini Dodoma. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...