AZANIA Benki inajivunia uzalishaji wa huduma kwa kila mmoja kwa wateja wake bila kujali dini, kabila na jinsia kwa faida na hasara kwa kuandaa futari pamoja na waislamu walioungana na wateja wa benki hiyo.

Akizungumza juzi katika hafla ya futari iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Benki hiyo, Rhimo Nyansaho alisema wameungana na waislam katika futari hiyo ikiwa ni sehemu yao ya kushirikiana na jamii.

Nyansaho alisema benki hiyo inasonga mbele kwa sababu ya michango ya jamii katika benki hiyo ndio maana kipindi cha mfungo wakaona ni sahihi kurudisha pato hilo kwa kufuturu na jamii yenye uhitaji kama watoto yatima na wengineo.

Mkurugenzi huyo alitumia fursa hiyo kuisifia benki yake kwamba wanatoa huduma bora na ndio maana faida inayoongezeka wanairudisha kwa jamii.Aliipongeza serikali kwa kuweka mazingira ya kushuka kwa riba katika benki mbalimbali ingawa wao walishashusha riba zao muda mrefu.

Mwakilishi wa wateja wa benki hiyo, Deogratius Kifumani aliipongeza benki hiyo kwa huduma zake inazotoa na kutoa wito kwa jamii kuelekeza mikakati yao ya kiuchumi huko.Kifumani alisema ubora wa huduma zao ndio maana inafanikisha matukio muhimu kama hayo katika jamii kwa kurudisha sehemu ya pato lao. 
Ofisa Masoko Mwandamizi wa Azania Bank, Othman Jibrea, akizunguma katika hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake pamoja na watoto yatima wa kituo cha Ijango Zaidia cha Sinza.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Azania Bank, Rhimo Nyansaho, akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake na kuwahusisha watoto yatima wa kituo cha Ijango Zaidia cha Sinza.
Sheikh Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Maulid Kidebe, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Azania Bank kwa ajili ya wateja wake pamoja na watoto yatima.
Sheikh wa Wilaya ya Ubungo, Shjeikh Maulid Kidebe. akiwaongoza wateja wa Azania Bank wakati wa futari iliyoandaliwa na benki hiyo iliyowahusisha watoto wa kituo cha watoto yatima cha Ijango zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya wateja wa Azania Bank wakipata futari iliyoandaliwa na benki hiyo na kuwahusisha watoto wa kituo cha yatima cha Ijango Zaidia cha Sinza jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...