Ubalozi wa Kuwait umekabidhi zawadi ya vifaa tiba katika Hospitali ya Wilaya ya Kigamboni ya Vijibweni vyenye thamani ya shilingi milioni 12 za kitanzania ikiwa ni utekelezaji wa mwanzo wa ushirikiano mzuri baina ya Kigamboni na Taifa la Kuwait. 

Akizungumza jana kwenye mapokezi ya vifaa tiba hivyo Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe.Mgandilwa ameshukuru kwa zawadi hizo alizozitoa Balozi wa kuwait ikiwa ni ahadi aliyoitoa alipotembelea Hospitalini hapo wiki mbili zilizopita. Mhe. Mgandilwa alisema kuwa matembezi ya Balozi wa Kuwait katika Hospitali ya vijibweni yalimfanya kubaini changamoto ya baadhi ya vifaa, hivyo kuahidi kurudi kabla ya mwezi wa ramadhani kuisha.

Aliesma kuwa Kuwait na Tanzania ni marafiki na kuna kila sababu ya kuendelea kusapotiana na kudumisha urafiki uliopo huku akimuomba Balozi wa Kuwait kuendelea kusaidia baadhi ya vifaa ambavyo ameahidi atavileta kama vile vitanda vya kung'olea meno vitakavyosaidia kuboresha huduma za afya kwa ubora zaidi.

"Naomba usiishie hapa kwa chochote utakaachona unaweza kusapoti kwenye sekta hizi tatu usisite kutusaidia na mimi kama Mkuu wa Wilaya naahidi kudumisha urafiki wetu" Alisema Mkuu wa Wilaya. Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Mhe. Jasem Al-Najem alisema zawadi alizozitoa ni mwanzo wa ushirikiano mzuri uliotokana na mapokezi mazuri aliyoyapata kipindi chote kutoka kwa Mkuu wa Wialaya ya Kigamboni pindi alipotembelea Wilayani kwake.

Aliongeza kuwa Ubalozi wa Kuwait umetoa Vitanza 3 vya watoto, vitanda3 vya kujifungulia kinamama, mashine za oksijeni, mabeseni 8 ya watoto waliozaliwa , mashine ya kutolea uchafu pindi mtoto anapokunywa maji machafu wakati wa kujifungua na vifaa vingine ili kuboresha huduma za afya zinazotolea na Hopsitali ya Vijibweni.

Balozi Jasem aliongeza kusema kuwa ataangalia namna atakavyoweza kusaidia kutoa mashine za moyo zilizoombwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni na kuahidi kuendeleza ushirikano uliopo na Kigamboni na Tanzania kwa ujumla. Aidha alisema kuwa Kuwait ina mpango unaojulikana kama Kuwait Blood Bank yenye lengo la kutunza damu salama hivyo atajitahidi kuhakikisha Kigamboni inakua miongoni mwa wanufaika wa mpango huo hususani Hospitali ya Vijibweni ambapo viataletwa vifaa vitakavyotumika kuhifadhia damu salama kwaajili ya kuokoa maisha ya Wananchi wa Tanzania.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mhe.Hoja Maabad alimshukuru Balozi wa Kuwait kwa zawadi alizozitoa na kumuomba kuendeleza urafiki na ushirikiano mzuri ulioanzishwa kwa manufaa ya wote.

Imeandaliwa na:
Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano
Halmshauri ya Manispaa ya Kigamboni
11/06/2018
 Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, leo tarehe 10/6/2018 amepokea ugeni wa Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jasem Al Najem.

Mapema akimkaribisha mgeni wake, DC Mgandilwa amemshukuru Balozi Najem kwa moyo wake wa upendo kwa  watanzania hususani wakazi wa Kigamboni. Ameeleza kuwa vifaa ambavyo vimetolewa ni vya zaidi ya Shilingi milioni kumi na moja na vinalenga kuondoa changamoto iliyokuwepo katika wodi za akina mama na watoto. 
Vifaa vilivyopokelewa ni pamoja na mashine za kusaidia wakati wa upasuaji, mashine za kusaidia kupumua, vifaa vya kupima moyo, vitanda vya watoto na beseni maalum kwa ajili ya akina mama wanaojifungua. 

DC Mgandilwa amesema kuwa nchi ya Kuwait ni miongoni mwa nchi ambazo ni marafiki wazuri wa Tanzania na kuwa Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kigamboni itaendeleza ushirikiano huo mwema. Kwa upande wake, Balozi Jasem Al Najem amewapongeza viongozi wa wilaya ya Kigamboni kwa ushirikiano mzuri ambao wamekuwa wakimpatia mara zote alipotembelea wilaya hiyo. 

Balozi Jasem ameeleza kuwa vifaa tiba alivyovikabidhi sio msaada bali ni zawadi kutoka kwa watu wa Kuwait kwenda kwa marafiki zao walioko Tanzania. 
Balozi Najem ameongeza kuwa huo ni mwanzo tu kwani baadhi ya vifaa tiba vingine vilivyoombwa na DC Mgandilwa atahakikisha vinapatikana na kuletwa ili kusaidia watu wa Kigamboni na watanzania kwa ujumla. 

Hafla ya kukabidhi vifaa tiba imefanyika katika hospitali ya  Vijibweni na baadae DC Mgandilwa alimkaribisha mgeni wake iftar iliyoandaliwa katika viwanja vya Msikiti wa Gaddafi uliopo Kigambobi.
Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa akipokea sehemu ya vifaa tiba kutoka kwa Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jasem Al Najem.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ushuhuda wa Tukio la ushirikina mjin Kigoma.

    Habar zenu Wadau
    Juzi shoga yangu alifukuzwa kazi hapa tukaelekezwa na rafiki yangu kwa mzee Kingwele anaishi Mpakan na Congo.

    Tulipatiwa huduma pale siku nne tuu.
    Siku ya pili na ya tatu tulivyokwenda nikashuhudia folen kubwa sana ya watu wenye shida mbalimbali ila idadi kubwa ni wanawake.

    Tukiwa pale kuna mteja mmoja ndio alikuwa anahudumiwa na Babu.

    Ndipo kwa mara ya kwanza kuona Babu akivuta msukule kupitia Mitambo yake.

    Ndugu wa yule mgonjwa walilia sana kwa furaha.

    Ikawa babu anahangaika na Madawa ili amrejeshe vizur akili yake aweze kuongea.

    Wakat tupo pale baadae nikaona tena Wagonjwa wengine wakitoa shukran zao kwa kumpa Babu zawad.

    Nilijaribu kudadisi kwa Wajukuu zake nikaambiwa.

    A) Mzee Mangi alikuwa na kesi ya Kuua lakin file la kesi yake lilipotea hivyo kesi ikafa na yule Afande aliyeshika file alipata ajali na amelazwa hospital

    B) Mama Omar alifanikiwa kurudiana na Mume wake aliyemtelekeza takriban miaka mitano.
    Mama huyu alihudumiwa na Babu kwa siku saba tu

    C) Ustadh Hussen nae alifanikiwa kupata utajir kwa njia nyepes tuu siyo kuua binadam bali kuchinja Mbuzi mmoja kwa Mwaka kila Tareh ikifika

    D) Nikaona ...... Akimkabidhi babu Solar baada ya kufanikiwa kuua ndugu.... Aliyekuwa akimsumbua Sana.

    E) Mama Zuwena alitoa sh... Ya shukran kwa Babu baada ya Mgahawa wake kujaza wateja sana na chakula hakilali.
    Hivyo dawa ya Mvuto wa biashara iliyochanganywa na .... Ilifanya kazi vizur.

    Note: Shoga yangu nae alirudishwa kazin baada ya wiki moja na hivisasa tupo Dar tumechukua likizo angalau tubadilishe Mazingira..

    Kiufupi huyu Babu anawajukuu zake ambao ndio huwa anawatuma kuchimba dawa na anachanganya na VISIMBA na mambo mengine anayoyajua yeye....

    Mmh! Najua kuna watakao toa Povu ila uhalisia ni kwamba Ushirikina/Uchawi upo na watu wanapata huduma mbali mbali wanafanikiwa ila watakaosema Uchawi haupo basi hao hawajapata matatizo.

    Namba za huyo Babu.
    (+255678134718) kwa ufafanuz zaid..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...