Na Frankius Cleophace Tarime.

Viongozi watatu Wanaotokan ana Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Nyamwaga Wilayani Tarime Mkoani Mara wamevuliwa wanachama na kupoteza sifa ya kuwa Viongozi kwa kukiuka Maadili ya uongozi pamoja na Katiba za Chama chao.

Mkutano Mkuu wa CHADEMA Kata ya Nyamwaga umewavua uanachama Viongozi hao akiwemo Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji Nyamwaga Getende Sagirai, Mjumbe wa Serikai ya Kijiji Koroso Sasi na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mchanchara Mniko Chacha

Lukas Ngoto ni Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Tarime Mkoani Mara akiongea na Waandishi wa habari amesema kuwa Mkutano Mkuu wa Chama ulioshirikisha Viongozi wa Wilaya umewasimamisha Viongozi hao kwa tuhuma mbalimbali.

Ngoto amesema kuwa Mwenyekiti wa serikalia ya Kijiji cha Nyamwaga natuhumiwa kwa kutumia vibaya madaraka yake huku baadhi ya Fedha zinazotokana na Mnara pamoja na Maji hazijulikani zimeenda wapi

Pia Ngoto ameongeza kuwa Mwenyekiti huyo amekuwa akikashifu chama hicho katika Vijiwe suala ambalo ni kukiuka kanuni ya Chama hicho.

“Sasa viongozi hawa watatu wamevuliwa uanachama na watapoteza sifa ya kuwa viongozi na tayari tumewateua baadhi ya vuongozi wa Muda wakati huo tukisubiri kufanya uchaguzi wa kuziba pengo na tunaenda kuandika barua kwa ajili ya kutaarifa Maofisa watendaji wa kata ili wasiwatambue” alisema Ngoto.

Jitiada za Kumtafuta Mwenyekiti huyo ili kuongelea juu ya kuvuliwa wanahama zimegonga Mwamba baada ya Simu yake ya Mkononi kuita bila kupokelewa.
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Lukas Ngoto akiongea na Waandishi wa habari kuhusu kuvuliwa uanachama kwa Viongozi hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...