Mwenyekiti
wa Jumuia ya Wazazi Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM
Dk. Edmund Mndolwa akipata maelezo kuhusu eneo lenye madini la Jumuiya
hiyo lililopo katika Kijiji cha Bigigi, alipokagua eneo hilo akiwa
katika ziara ya kikazo mkoani Singida, jana. Anayempa maelezo ni Katibu
wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Singida Mjini Ali Balo (Wapili kushoto)
na kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati Sosthenes
Masola. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi na
Mjumbe wa NEC- CCM Christina Joramu na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya
hiyo kwa upande wa Zanzibar Haidar Haji abdallah. Dk. Mndolwa ameagiza
uongozi wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Singida kuharakisha kulitafutia
leseni na kuliwekea vigingi vya mipaka eneo hilo.
Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa akisalimia baadhi ya
viongozi wa Jumuiya hiyo baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Singida,
kuanza ziara ya kikazi mkoani humo, jana.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Singida Mashigani Kija akisoma taarifa ya jumuiya hiyo mbele ya Dk. Mndolwa
Mwenyekiti
wa Jumuia ya Wazazi Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM
Dk. Edmund Mndolwa akipata maelezo kuhusu eneo lenye madini la Jumuiya
hiyo lililopo katika Kijiji cha Bigigi, alipokagua eneo hilo akiwa
katika ziara ya kikazo mkoani Singida, jana. Anayempa maelezo ni Katibu
wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Singida Mjini Ali Balo.PICHA ZOTE NA
BASHIR NKOROMO
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...