Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dk. Edmund Mndolwa akipata maelezo kuhusu eneo lenye madini la Jumuiya hiyo lililopo katika Kijiji cha Bigigi, alipokagua eneo hilo akiwa katika ziara ya kikazo mkoani Singida, jana. Anayempa maelezo ni Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Singida Mjini Ali Balo (Wapili kushoto) na kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati Sosthenes Masola. Kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi na Mjumbe wa NEC- CCM Christina Joramu na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kwa upande wa Zanzibar Haidar Haji abdallah. Dk. Mndolwa ameagiza uongozi wa Jumuiya ya Wazazi mkoani Singida kuharakisha kulitafutia leseni na kuliwekea vigingi vya mipaka eneo hilo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa akisalimia baadhi ya viongozi wa Jumuiya hiyo baada ya kuwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Singida, kuanza ziara ya kikazi mkoani humo, jana. 
 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Singida Mashigani Kija akisoma taarifa ya jumuiya hiyo mbele ya Dk. Mndolwa
 Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Dk. Edmund Mndolwa akipata maelezo kuhusu eneo lenye madini la Jumuiya hiyo lililopo katika Kijiji cha Bigigi, alipokagua eneo hilo akiwa katika ziara ya kikazo mkoani Singida, jana. Anayempa maelezo ni Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Singida Mjini Ali Balo.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...