Shirika la PELUM Tanzania kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeanza zoezi la kutoa hatimiliki za kimila zipatazo 747 kwa wananchi wa vijiji vitano ambao wamefanyiwa mpango wa matumizi ya ardhi kupitia mradi wa ushiriki wa wananchi katika kusimamia sekta ya kilimo ulio chini ya watu wa marekani 

Hatimiliki hizo zinatarajia kunufaisha wanawake 250, wanaume 385, wenza wenye ushiriki wa pamoja 97 pamoja na maeneo ya Taasisis 97 toka vijiji vya Usokame, Ugesa, Magunguli, Isaula na Makungu

Simon Mbago Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Mufindi anayesimamia zoezi hili, mbali na kulishukuru Shirika la PELUM Tanzania kwa kufanya nao kazi kwenye vijiji hivyo amesema kufanyika kwa mpango wa matumzi ya ardhi hadi kufikia utoaji wa hatimiliki imesaidia kutekeleza majukumu ya Halmashauri ambayo yalipaswa kutekelezwa na Halmashauri husika.

“Ni jukumu la kila Halmshauri kuhakikisha inatenga fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo ili kufanyia vijiji vyake mpango wa matumizi ya ardhi lakini uwepo wa mashirika binafsi kutekeleza jukumu hili ikiwemo PELUM Tanzania imesaidia kwa kiwango kikubwa kuchochochea maendeleo katika Halmashauri yetu.”

Hivyo basi uwepo wa hatimiliki hizi tunazogawa zitasaidia wananchi wa Halmashauri yetu kuzitumia kuomba mikopo kwenye taasisi za fedha kwa kuweka dhamana maeneo yao jambo ambalo wamekuwa wakilisubiri kwa kipindi kirefu ili kuwawezesha kufanya shughuli nyingine za kiuchumi kupita fedha watakazopata.
Evance Kibasa Mwananchi kutoka kijiji cha Usokame akiwa na Hatimiliki yake ya kimila baada ya kukabidhiwa.
Mmoja wa wananchi toka kijiji cha Usokame akikabidhiwa hatimiliki ya kimila na Afisa Ardhi wa Halmashauri ya wilaya ya Mufindi Simon Mbago
Asafu Mgelekwa na Mkewe Atuganule Lunyungu wakiwa na hati yao yenye umiliki wa pamoja
Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Ugesa wakiwa na hatimiliki zao za kimila

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...