Image may contain: 12 people, indoor
Na Mwandishi wetu, Washington, DC
Nimeona nikae chini niipitie maandiko ya mhenga moja aliyeandika habari ya DISCO iliyokua na kichwa cha habari "WAHENGA TULITESA SANA ENZI ZETU DISCO LA MCHANA (BOOGIE) NA MA-DJ WAKALI!!!" mwandishi wa habari hiyo amejitahidi sana kuelezea kwa mapana ya ufahamu wake jinsi gani alivyoujua muziki wa Disco wa enzi zile waliwemo maDj wake.

Mimi nimeamua kuweka sawa baadhi ya mambo Dj Kalikali yeye alishapiga muziki YMCA wakishirikiana na Dj Niga Jay na kuna wakati pia walipiga pamoja na Dj John Peter Pantalakisi na muda mwingi John Peter Pantalakis walikua wakishirikiana na Dj Chogy Sly Dico la Born City na kuna kipindi fulani Dj Kalikali alikua Dj wa Disco la RSVP ambalo Mbowe walianzisha tawi la DICO  katika hotel ya New Africa ghorofa ya saba.
Image may contain: 5 people, including Richie Dillon, people smiling, people standing and outdoor
Muziki wa Disco unasafari ndefu maDj wengi wa zamani walikua wanamuziki wa bendi na baadae kubadili mwelekeo na kuwa maDj kwa mfano Dj Sweet Francis na Dj Addy Sally chimbuko lao walitokea kwenye bendi na baadae miaka ya 1970 wakahamisha mawazo yao na kuwa maDj wakati huo kukiwa na Disco la Banda Beach, Sea View na madisco mengine Kilimanjaro Hotel Summit

Nataka nikupe historia ya musiki na disco theque.Africana Gogo Disco lilianza mwaka 1971 na aliyeanza kupiga disco hapo ni Bhoka Wilson (Mzimbabwe) wakati ule ikiitwa Southern Rhodesia naye alikuwa cabbaret singer Simba Grill Kilimanjaro hotel. August 1972 Dj Sweet Fransis akawa Dj hapo mpaka Nov.1973 kisha akawa Dj. Judy Kingui (Msouth Africa ambaye alikuwa mkewe Kingui aliyekuwa mwenye The Rifters Band. Judy alikuwa Dj.hapo Gogo Disco mpaka 1975.

Katika historia ya muziki wa disco Tanzania ambayo inabeba Madj wengi wengine wakiwa wametangulia mbele ya haki 
Disco la XTC ambalo maDj hawa wamepitia David , Lawrance , Pailonga, TNT Jackson

Disco la Valentinos/Continental haliwezi kutajwa bila ya watu hawa Ibrahim G ,Camal, Mr A, Salai, Meb, Guru, Sabry Kube

Disco la Rungwe 110 halijakamilika bila ya watu hawa Chogy Sly JP Pantelakis, Roma Pop Juice, Amon Washington, Agib Show, Ibony, Ntimizi, Bhester, Kim and the boyz, John Bure na wengineo
Image may contain: 5 people, including Muhidin Issa Michuzi, people smiling, people standing, stripes, beard and outdoor
Dj Sweet Francis jina kamaili ni Francis James Bundala,mwaka 1964 alianzisha bendi iliyoitwa The Screemers na Dj Sweet Francis akiwa mwimbaji(singer) hapo ndipo alipopewa jina la SWEET baada ya kusikia sauti yake na jinsi alivyokuwa akiimba iliwakuna sana na wakawa wanasema "YOUR VOICE IS SO SWEET " na ndiyo hapa akawa anaitwa Sweet. Hiyo ni hapa Dar.Bendi The Screamers ilidumu muda mfupi. Mwaka 1965 alianzish a bendi nyingine ya watu 5 wakaiita The Hot Five wakawa wanapiga bugi kila Jumapili mchana hapo Arnatoglo hall Mnazi mmoja. Wakawa wanashindana na bendi ilikuwa inaitwa The Flamming Star.

 Mwaka 1967 June The Hot Five ikavunjika. 1967 Sept. Dj Sweet Francis na aliyekuwa Solo guitarist wakaanzisha bendi nyingine wakapata watu wengine 3 ambao walianza kuwafundisha ambao walikuwa mpiga bass, mpiga rythym na drummer. Bendi wakaiita The TONICS. Mwimbaji- Sweet, Solo- Michael Jackson, Rythym- Green Jackson. Bass- John Morand na Drums- Charles Alowasa. 

Baada ya mazoezi makali mwezi November1967 wakaapata mkataba wa kupiga muziki kila siku hapo Splendid Hotel iliyokuwa inamilikiwa na mtaliano aliyeitwa MOSKA mtaa wa Samora zamani ukiitwa Independence Ave.

Siku moja wakati wanapiga muziki jamaa mmoja ambaye hawakuwa na mazoea naye akaja kwenye stage akaomba apige bongos wakamruhusu, wakati Dj Sweet Francis anaimba na yule jamaa akawa amapiga bongos vizuri sana Dj Sweet Francis akawaambia wenzake kuwa anafaa kuwa drummer lakini wenzake walimkatalia na baada ya kuwasihi sana walikubali kwa sharti kuwa amfundishe kupiga drums mpaka ajue. 
Image may contain: 10 people, including Ahmed Chande and Peter Moe, people smiling, people standing and outdoor
Baada ya kumfundisha kwa muda mfupi akaona ameelewa na baada ya kumpa nafasi kwenye stage alipiga drums na wenzangu wakamfurahia, huyo alikuwa anaitwa Adam Salehe Mwambile (R.I.P.) na tangu siku hiyo Dj Swett Francis akamwambia kuazia leo utaitwa ADDY SALLY,  ilikuwa mwezi April 1968, hilo ndiyo lilikuwa chimbuko la ADDY SALLY. 

May 1968 mkataba ulimalizika hapo Splendid  wakaamua kwenda mikoani.Wakati wote huo Dj Sweet Francis alikuwa mfanyakazi wa NPF sasa ni NSSF.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...