*Wazungumzia namna wanavyofanya tafiti, kutoa huduma bora

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
MKUU wa Idara ya Hematolojia, Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Program ya Selimundu katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili(MUHAS) Profesa Jullie Makani amesema wapo katika mchakato wa kutoa huduma ya kutibu Selimundu kwa Kupandikiza ute wa Mifupa

Prof.Makani amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Selimundu Duniani yaliyofanyika katika Hospitali ya Mlaganzila ambapo amesema kwa sasa wapo katika mchakato wa mazungumzo na yakikamilika wanatarajia kuanza kutibu Selimundu kwa kutumia tiba ya Kupandikiza Ute wa mifupa kwa mgonjwa.

"Zipo njia mbili zinazotumika kutibu Selimundu.Njia ya kwanza ni kwa kutumia Hydroxyurea na ndio ambayo tunaitumia hapa nchini.Njia ya pili ni ya kutibu kwa kupandikiza ute wa mifupa ambayo kitalaam inafahamika Bone Marrow Transplant,"amefafanua.

Alipoulizwa ni lini wataanza kupandikiza ute wa mifupa kwa mgonjwa wa Selimundu katika hospitali hiyo amejibu wanatarajia kuanza mwakani iwapo mchakato utakwenda vizuri hata.Pia amesema haijafahamika gharama ya kutibu kwa kupandikiza ute wa mifupa itakuwa kiasi gani na ndio mazungumzo ambayo wanaendelea nayo kufanya.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MuHAS) Profesa Appolinary Kamuhabwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Ugonjwa wa Seli Mundu yaliyofanyika kwenye Chuo Kikuu hicho Kampasi ya Mloganzila leo na kushirikisha Madaktari Bingwa, Watafiti wa Magonjwa na Tiba mbalimbali na wauguzi, Profesa Kamuhabwa amesema chuo hicho mpaka sasa ina miradi ya utafiti wa magonjwa mbalimbali pamoja na tiba inayofikia 92.
Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS)akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Seli Mundu yaliyofanyika katika Chuo hicho Kampasi ya Moganzila leo.Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS) akizungumza katika maadhimisho ya siku ya Seli Mundu yaliyofanyika katika Chuo hicho Kampasi ya Moganzila leo.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MuHAS) Profesa Appolinary Kamuhabwa katikati ,Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS) kushoto na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud wakifuatilia baadhi ya taarifa za tafiti zilizokuwa zikionyeshwa kwenye Projekta. 
Baadhi ya wataalamu na madaktari mbalimbali wakiwa katika maadhimisho hayo. 
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud akitoa shukurani zake wakati wa maadhimisho hayo mara baada ya kutolewa kwa taarifa mbalimbali za kiutafiti katika chuo hicho.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MuHAS) Profesa Appolinary Kamuhabwa katikati ,Profesa Julie Makani Mkuu wa Idara ya Hematolojia , Uwekaji wa Damu na Mtafiti Mkuu wa Programu ya Seli Mundu (MuHAS) kushoto na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Huduma za Hospitali Profesa Said Aboud wa pili kutoka kushoto pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Udahili na Uzamivu (MuHAS) Emmanuel Balondya kushoto wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari Bingwa, Wataalam na Watafiti wa chuo hicho.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...