KAMPUNI ya Aon kupitia Minet imezindua rasmi JH Minet Tanzania ikiwa ni mwendelezo wa safari iliyoanza 1998 ikiwa inatoa huduma za bima pamoja na mafao.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Minet Group Joe Onsando amesema kuwa kampuni hiyo mpya itakuwa chini Aon na hakuna kazi itakayopotezwa baada ya mabadiliko hayo.

Amesema  kuwa Minet  ni kampuni inayoaminika  kote Afrika na nje ya bara hilo na wafanyakazi wa Aon ambayo sasa itajukulikana Minet katika nchi hizo na viongozi wao ambao wana ujuzi katika masuala ya viwanda wataendelea kuwa nafasi kama watendaji katika utoaji wa huduma.Onsando ameeleza kuwa mwaka 1997  kampuni hiyo ya  JH Minet ilibadilishwa na kuwa Aon Minet na wanaendelea kujenga uchumi imara Afrika na itaendelea kuwa sehemu ya Aon katika utendaji kazi wao.

Onsando amefafanua kuwa huduma zinazotolewa na kampuni hiyo hazitabadilika katika sekta zote kama vile kilimo, madini na mawasiliano.Pia amesema wanafurahishwa na namna uwekezaji unavyoendelea na kukua barani Afrika na wataendelea kutoa huduma bora kwa wateja wao kwa sasa na baadaye.

Viongozi wa kampuni ya Minet wakizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu uamuzi wa kufanya mabadiliko ya jina la kampuni hiyo.
Baadhi ya viongozi wa kampuni inayojihusisha na masuala ya bima na mafao ya MINET wakisalimiana na baadhi wageni waalikwa waliofika kushuhudia mabadiliko ya jina la kampuni hiyo. 
Baadhi ya viongozi wa kampuni inayojihusisha na masuala ya bima na mafao ya MINET wakisalimiana na baadhi wageni waalikwa waliofika kushuhudia mabadiliko ya jina la kampuni hiyo.
Wageni waalikwa walioshiriki uzinduzi wa jina jipya la Kampuni ya MINET wakifuatilia tukio hilo ambalo limefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuria na watu mbalimbali ndani na nje ya Tanzania.

Mwanamuziki maarufu barani Afrika Vyone Chaka Chaka akisakata rumba na baadhi ya wageni waalikwa kwenye tukio la uzinduzi wa jina jipya la Kampuni ya MINET.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...