Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Katika kuadhimisha  ya siku ya mtoto wa Afrika leo kikundi cha Beauty with Brain kwa kushirikiana naSerena Hotel  wamemtoa msaada wa vitu mbalimbali kwa kituo cha watoto wanaoishi  kwenye mazingira cha serikali kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam. 

Beauty with Brain pamoja na Serena waliweza kukabidhi vyakula, mafuta ya kupikia, masweta ya watoto, rangi na gypsum kwa ajili ya ukarabati wa sehemu ya kulia chakula, vitabu, nguo na baadhi ya vitu vingine.

Akizungumza ma wanahabari baada ya kukabidhi kwa vitu hivyo, Mwenyekiti wa Beauty With Brain Teddy Mapunda alisema kuwa lengo kuu la kuwasaidia watoto hao ni kuwafanya wajisikie wanafamilia zinazowapendà  na kuwajali pia.

Teddy amesema, katika siku ya leo wamekuja na zawadi mbalimbali kwa watoto hao ikiwemo vitabi vya kujisomea, masweta 71 kwa watoto wote na pia  nguo na viatu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika.

Kikundi hicho kimeweza kushirikiana bega kwa bega na Serena Hotel na kufanikisha kupatiwa kwa zawadi hizo kwa watoto hao ambapo Mkurugenzi wa Rasilimali Wa Serena Hotel Sophia Mketo amesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu wameamua kujumuika pamoja na watoto wa kituo cha Kurasini na wameona wanahitaji sana mchango wao.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Umoja wa wanawake cha Beauty with Brain cha jijini Dar es Salaam,Teddy Mapunda (wa pili kulia) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vitabu mmoja kati ya watoto wanaolelewa katika Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Serikali kilichopo Kurasini,jijini Dar es Salaam,wakati kinamama hao kwa kushirikiana na Hoteli ya Serena, walipotembelea kituo hicho leo asubuhi na kukabidhi Vyakula, Ndoo za rangi, Gipsum Board, Masweta ya watoto wote 71, nguo na viatu, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika. Picha Zote na Nasma Mafoto
Mazungumzo kabla ya kukabidhi msaada huo
Kina mama wa Beauty With Brain wakikabidhi sehemu ya msaada huo kwa watoto wa kituo chaWatoto Yatima ikiwa ni katika kuadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Umoja wa wanawake cha Beauty with Brain cha jijini Dar es Salaam,Teddy Mapunda akizungumza na wanahabari baada ya kukabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaoishi kwenye kituo cha watoto yatima Kurasini ikiwa ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika leo Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu wa Hoteli ya Serena, Sophiaakizungumza na wanahabari baada ya kukabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaoishi kwenye kituo cha watoto yatima Kurasini ikiwa ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika leo Jijini Dar es Salaam
Msimamizi wa Kituo ya Yatima cha Kurasni Beatrice Mgumiro, akiwashukuru kikundi cha Beauty with Brain pamoja Serena Hotel kwa kuwakumbuka watoto hao wanaoishi katika kituo cha watoto yatima Kurasini.
Baadhi ya wafanyakazi wa Hotel  Serena Hotel wakiwa katika picha ya pamoja.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...